Halmashauri ya wilaya ya Kyela imetoa semina kwa wasimamizi na waandikishaji wa wananchi katika daftari la wapigakura, semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri na katika kata ya Ipinda leo tarehe 04/10/2019.
Akizungumza na watumishi wasimamizi, Katibu tawala wa wilaya ya Kyela, Mhe. Godfrey Kawacha amesema, Kazi hii si ngumu sana, ila inahitaji umakini wa hali ya juu ili kutoa haki ya kujiandikisha katika daftari ya mpiga kura kwa kila mwananchi.
Aidha amewataka watumishi hao kwenda kutekeleza, maagizo yote yatakayotolewa na wawezeshaji wa semina.
Zaidi ya watumishi 400 wameapishwa leo kwa maandalizi ya kuanza kazi ya kuwaandikisha wananchi katika daftari la mpiga kura, linaloandaliwa kwa ajiri ya uchaguzi wa viongozi wa serikali ya mitaa.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa