Afisa elimu mkoa wa Mbeya ndugu Ernest Hinju, amefanya kikao kazi tarehe 11/07/2023, katika viwanja vya shule ya msingi Nkuyu hapa wilayani Kyela.
Kikao kimeshirikisha Viongozi na walimu, akiwemo Afisa taaluma Mkoa ndugu, Kaniugu, Afisa elimu (W) ndugu, lydia Herbert, Afisa elimu Msingi (W) ndugu, Rowllence B.Kabuje, Maafisa taaluma (W), Maafisa elimu kata, Wakuu wa shule, walimu wakuu, pamoja na walimu wawili mahili wa masomo 6 katika ufundishaji.
Akizungumza katika kikao hicho Afisa elimu Mkoa ndugu Ernest Hinju amesema;
Lengo la kufanya kikao hicho ni kujadiliana mikakati ya kuinua taaluma katika mkoa wetu wa Mbeya, kufanya tathimini ya matokeo ya mtihani wa "MOCK" kanda kwa darasa la saba 2023.
"Ili kupata nafasi ya mkoa au wilaya katika taaluma, hesabu ya matokeo kwa mitihani 5 hufanywa, yaani mtihani wa darasa la 4, 7, kidato cha 2, 4 na 6 ili kupata wastani, hivyo hutuwezesha kujua nani anashika nafasi ya kwanza, Idara ya Elimu sekondari ni lazima wahusike katika kufanya tathimini ya matokeo" amesema ndugu Ernest Hinju.
Aidha amesema, amekuwa akifanya vikao kazi kwa kila halmashauri za Mkoa wa Mbeya, ili kuweka mikakati ya kupandisha Mkoa kitaaluma.
Pamoja na hayo, amewataka viongozi, walimu kudumisha upendo katika sehemu zao za kazi ili kuweka akili sawa na hatimae kuinua taaluma kwa wanafunzi wanaowafundisha.
Ametoa pongezi kwa Mkoa wa Mbeya kwa kuendelea kushika nafasi ya 3 Kitaifa, na amesisitiza upendo na mshikamano baina ya watumishi kwa lengo la kuinua taaluma ndani ya Mkoa.
"Mkoa wetu wa Mbeya umekuwa ni mfano wa kuigwa katika elimu na usimamiaji mzuri wa miradi kwa mikoa mingi nchini, na hata mikoa mingine imekuja kujifunza kwetu" Amesema Afisa elimu mkoa.
Nae Afisa elimu msingi (W) ndugu, Rowllence B. Kabuje alitoa tathmini ya matokeo ya mtihani wa darasa la 7 "MOCK" kanda, inayoshirikisha mikoa 5, wilaya ya Kyela ikiwa imeshika nafasi ya 18 kati ya halmashauri 27 za kanda.
Ndugu Ernest Hinju ataendelea na ziara za kufanya kikao kama hiki katika halmashauri nyingine za Mkoa wa Mbeya.
Mwisho.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa