• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Asanteh Rais wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa Vifaa Tiba Mitambo Katika Hospitali Ya Wilaya Kyela

Imewekwa Kwenye: February 15th, 2023

Waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya wilaya Kyela wametoa shukrani zao za dhati, kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuiwezesha Hospitali ya wilaya ya Kyela, kununua vifaa tiba vya kisasa vyenye thamani ya shilingi 376,000,000/= ikiwa ni pamoja na ununuzi wa mitambo katika hospitali hiyo.

Shukrani hizi zimetolewa katika ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo, kwa robo ya 2 ya mwaka 2022/2023. Waheshimiwa madiwani wamesema kwa sasa Hospitali ya wilaya imekuwa na vifaa tiba vya kisasa na vya kutosha kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali bila usumbufu wowote.

Akiongea na waheshimiwa madiwani wa kamati ya Elimu na Afya, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Lembris Leizer amesema,

Baada ya mapokezi ya fedha hizo, Halmashauri iliandaa mahitaji ya kila kitengo katika hospitali ya wilaya, na kununua vifaa kulingana na mahitaji ya kitengo.

"stationary bicycle" mashine ya kuwasaidia waliopata kiharusi na kuleta mzunguko wa damu kwenye mwili, "Microscope olmpus cx23" inayosaidia kutambua wadudu wasioweza kuonekana kwa macho, Mashine za magonjwa yote ya meno, Mafriji kwa ajili ya kutunzia damu, mitambo ya kufulia nguo pamoja na vifaa vingine vingi vimemunuliawa.

Aidha waheshimiwa madiwani kwa kupitia kamati zao za kudumu wameweza kupitia na kukagua miradi ifuatayo;

Kikundi cha wajasiriamali bodaboda kikundi kilichokopeshwa fedha na halmashauri, ujenzi wa vyumba 17 vya madarasa katika shule ya sekondari Mwakilima, shule ya msingi uhuru, shule ya sekondari Kafundo, shule ya msingi Ikulu, pamoja na  shule ya sekondari Lubele.

Ujenzi wa bweni la wanafunzi shule ya sekondari Kyela coal mine.

pamoja na miradi hiyo kamati hizo zimeweza kutembelea ujenzi wa bweni la wanafunzi katika shule ya Kyela coal mine, ujenzi wa kituo cha afya kata ya Itope, ujenzi wa zahanati ya Itekenya katika kata ya katumba songwe, ujenzi wa shule mpya ya sekondari Ibanda, ikiwa ni pamoja na jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya Njisi.

Ujenzi wa bweni la wanafunzi shule ya sekondari Nyasa lakeshore.

Aidha katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri Katule G. kingamkono alijitolea kuwa mlezi wa Jackline Mshana na kuahidi kumlipia bima ya NHIF  mwanafunzi  mwenye mahitaji maalumu, katika shule ya msingi Isaki, 

Hata hivyo Mhe. Mwenyekiti ameahidi kutoa mifuko 30 ikiwa mifuko 10 kwa ujenzi wa Shule mpya ya ibanda,  mifuko 10 kwa ujenzi wa kituo cha Afya Itope na mifuko 10 kwa ujenzi wa zahanati ya Itekenya. Wakati huo huo, Kaimu Mkurugenzi aliahidi kupeleka mifuko 10 ya simenti katika ujenzi wa zahanati ya Itekenya kwa niaba ya wataalam.

Mwisho pongezi nyingi zimetolewa kwa wataalam kwa kusimamia na kutekeleza vyema maagizo yanayotolewa na viongozi na hata kuifanya miradi mingi ya maendeleo kukamilika kwa wakati na viwango vikubwa.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa