• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Balaza La Mwaka La Waheshimiwa Madiwani Lafanyika Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: September 10th, 2024

Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkono ameongoza mkutano wa Baraza la kufunga Mwaka 2023/2024 la Waheshimiwa madiwani, katika ukumbi wa mikutano wa Halmshauri tarehe 09/09/2024.

Mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri Bi. Flora A. Luhala, Katibu tawala (W) Bi. Sabrina Houmud, taasisi mbalimbali za Serikali, Viongozi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), wataalam kutoka ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, pamoja na Wananchi.

Aidha katika Baraza Hilo umefanyika uchaguzi wa kumchagua Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya ya Kyela, ambapo, Mhe. Ambakisye Njerekela, ameibuka mshindi kwa kura za wajumbe 36 waliopiga kura.
Pia kulikuwa na uundwaji wa kamati za kudumu za Baraza kwa Mwaka 2024/2025, ikiwemo kamati ya Elimu na Afya, kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira,  kamati ya Lishe, kamati ya Maadili na kamati ya Uongozi Fedha na Mipango.

Akizungumza kwa niaba ya Mhe. Mkuu wa wilaya ya Kyela, Katibu Tawala (W) Bi. Sabrina Houmud,  amemshukuru  Mhe. Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za  kuanzisha na kuendeleza miradi ya maendeleo wilayani Kyela.

Pamoja na hayo Bi. Sabrina amempongeza Mhe. Ambakisye Njerekela kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya ya Kyela, pia amesisitiza kuendelea kudumisha ushirikiano uliopo baina ya Wanakyela.

Sambamba na hilo amewashukuru Waheshimiwa madiwani, kwa ushirikiano mzuri waliouonesha wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru, uliopokelewa tarehe 28/08/2024, wilayani Kyela.

Kuelekea katika uchaguzi mdogo wa Serikali za mitaa utakaofanyika tarehe 27/11/2024 Bi. Sabrina Houmud, amewaomba Waheshimiwa Madiwani na wataalam mbalimbali kuendelea kutoa elimu na ushirikiano ili kuhakikisha elimu ya kujitokeza kupiga kura inamfikia kila mwananchi.

Awali Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya ya Kyela Mhe. katule G .Kingamkono, amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Kyela.

Hata hivo Mhe. Katule ameendelea kutoa ufafanuzi wa utekelezaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii katika Halmshauri ya wilaya ya Kyela  kwa mwaka wa fedha 2023/2024, ikiwemo ukusanyaji wa mapato kwa 133%.

Akitoa salamu kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), Katibu mwenezi wa Chama Ndg. Emmanuel Mwamulinge, amewapongeza waheshimiwa Madiwani na wataalam kwa ushirikiano mzuri na Chama Cha Mapinduzi na kufanikiwa kiendelea kuleta maendeleo wilayani.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa