Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya Mhe.Tobiath Mwamkonda ameongoza mkutano wa Baraza tarehe 9.2.2026 katika ukumbi wa mikutano
Akizungumza kwenye mkutano huo Mhe.Mwenyekiti amempongeza Mkurugenzi Mtendaji na ofisi yake kwa ujumla kwa usimamizi mzuri wa fedha zinazoletwa na Serikali ya awamu ya sita kwa ajili utekelezaji mbalimbali wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela.

Mhe.Mwenyekiti amempongeza Mkurugenzi kwa kufikisha 61% za ukusanyaji mapato ndani ya robo ya pili.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe.Josephine Manase amewataka madiwani kutembelea na kukagua miradi inayotekelezwa kwenye kata zao ili kujua changamoto na namna huduma zinavyotolewa.

Mhe.Manase ameongeza kwa kuwataka madiwani wahamasishe Wazazi kupeleka watoto shule pamoja na kutoa elimu kwa Wazazi hao juu ya umuhimu wa kuchangia chakula ili watoto wapate chakula pindi wawapo shuleni.
Aidha Mkuu wa Wilaya amewataka madiwani kutoa elimu kwa Wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na mfuko wa bima kwa wote,huduma hiyo inatolewa kwa TSH.150,000/= kwa kaya moja yenye watu 6.Bima hiyo itasaidia kupata matibabu wakati wowote kwa haraka.

Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa