Halmashauri ya wilaya ya Kyela imetenga kiasi cha shilingi 403,000,000/= ikiwa ni mapato yake ya ndani kwa ajiri ya ujenzi wa kituo cha Afya katika kata ya Ngonga hapa wilayani Kyela.
Haya yamezungumzwa leo tarehe 20/09/2021 na Mkuu wa wilaya ya Kyela, mheshimiwa Ismail Mlawa alipokuwa akizindua ujenzi wa kituo hicho cha afya mara baada ya kushiriki katika kufanya kazi ya uchambji wa msingi, kusogeza tofali pamoja na kusomba mchanga. Shughuli ambazo zimefanywa na wananchi, viongozi pamoja na wakuu wa idara mbalimbali na vitengo kutoka halmashauri ya wilaya.
Aidha Mkuu wa wilaya huyo, amewatia moyo wananchi kuzidi kujitoa katika maendeleo ya mradi huo, ikiwa ni pamoja na kuzidi kuchangia nguvu kazi pamoja na fedha, ambapo amewaahidi kwamba atasimamia fedha zote zitakazotolewa na Serikali pamoja na wananchi, ili kuhakikisha hakuna shilingi itakayoibiwa katika ujenzi huo. Aidha amesema atachangia shilingi 500,000/=. Na pesa hiyo itawekwa katika akaunti mapema kesho tarahe 21/09/2021.
Pia alimuagiza Kaimu Mkurugenzi ndugu Kenneth Nzilano kuleta trekta la halmashauri, ili kusaidia shughuli za kusogeza mchanga na tofali eneo la ujenzi.
Aidha katika hafla hiyo, Mbunge wa jimbo la Kyela Mheshimiwa Ally Mlaghila Jumbe, amewaahidi wananchi hao kuwanao bega kwa bega katika kusaidiana kazi za ujenzi wa kituo hicho cha Afya hadi kitakapokamilika, na amesema atachangia mifuko 200 ya simenti katika ujenzi huo.
Pongezi nyingi zilitolewa kwa wakuu wote wa Idara na vitengo waliojitokeza katika kusaidia uhamasishaji wa ujenzi wa kituo cha Afya Ngonga, kwa kujitolea kuchimba msingi wa moja ya jengo linaloanza kujengwa kwa sasa.
Hadi sasa wananchi wamechangia shilingi 18,000,000/= tofali 120,000 zenye thamani ya shillingi 12,000,000/= pamoja na nguvu kazi.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa