Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za mitaa (LACC),imeridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Kyela.
Kamati imeridhishwa na miradi yote waliyoitembelea katika ziara yao ya tarehe 25/04/2022 na kupokea taarifa ya miradi hiyo. Miradi iliyotembelewa ni pamoja na mradi wa kituo cha afya Ipinda na mradi wa ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika hospitali ya wilaya ya Kyela.
Kaimu mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mheshimiwa Boniface Butondo amesema, amefurahishwa sana na umoja uliopo baina ya viongozi wa wilaya, na hata kusababisha usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Kyela.
Aidha Mheshimiwa Butondo alitoa baadhi ya ushauri na maagizo kwa viongozi ikiwemo, uwekaji wa uzio kuzunguka kituo cha afya Ipinda, ukarabati wa baadhi ya majengo katika hospitali ya wilaya ya Kyela, ukarabati wa jengo la wodi la wanaume katika kituo cha afya Ipinda. Ila aliwaomba TAMISEMI kusaidia fedha za ukarabati huo.
"Naomba niwashauri kuweka gata za maji ili kuvuna maji ya mvua pamoja na kulinda kuta za majengo zisichafuliwe na maji ya mvua" alisema mhe. Butondo.
Mwisho Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkono, alisema wamepokea maagizo yote na ushauri uliyotolewa na kamati na kuahidi kuanza kuyashughulikia utekelezaji wake kwa haraka. Mheshimiwa mwenyekiti aliyazungumza haya wakati akihojiwa na waandishi wa habari.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa