Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI, kifua kikuu, dawa za kulevya na magonjwa yasiyopewa kipaumbele yafanya ziara wilayani Kyela tarehe 21/09/2021.
Akizungumza kwa niaba ya waheshimiwa Wabunge wengine Mwenyekiti wa kamati hiyo Mheshimiwa Fatma Hassan Taofiq amesema kwamba, wameamua kuja kutembelea mkoa wa Mbeya hususani wilaya ya Kyela ili kuja kufahamu ni kwa jinsi gani mkoa wa Mbeya na Wilaya zake wanasimamia zoezi la kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Aidha, Mheshimiwa Mwenyekiti amewaagiza viongozi wote hapa wilayani Kyela kutoa elimu juu ya maambukizi mapya ya ugonjwa wa UKIMWI. Kwani takwimu zinaonesha kuwa, wilaya ya Kyela maambukizi yanazidi kupanda kwa kasi zaidi ukilinganisha hali ilivyo kwa nchi nzima. Pia aliwataka viongozi na waratibu, kutengeneza kampeni mbalimbali za kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI, Pia aliwasihi kutoa elimu juu ya tohara kwa wanaume kwani imethibitika kwamba kwa 60% tohara kwa wanaume hupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Kamati ya Bunge ya UKIMWI, kifua kikuu, dawa za kulevya na magonjwa yasiyopewa kipaumbele iliweza kutembelea Hospitali ya wilaya ya Kyela na kituo cha afya Ipinda na kuzungumza na wataalamu wa afya kwa lengo la kufahamu shughuli hizi zinavyoratibiwa hapa wilayani Kyela.
Shughuli zote za UKIMWI zinafadhiliwa na HJF Medical Reseach International kupitia mradi wa Walter Reed Program Tanzania kwa mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa