Kamati ya siasa ya Mkoa ikiwa inamsikiliza eng.Mohamed A.Muanda kutoka TARURA, ambae ni mtaalam wa ujenzi wa barabara.
Kamati ya siasa ya mkoa wa Mbeya imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo hapa wilayani Kyela. Ziara hii imefanyika tarehe 16/02/2022.
Miradi iliyotembelewa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa barabara za rami Kyela mjini, ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika hospitali ya wilaya ya Kyela, ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Itunge kituo kinachojengwa kwa fedha za tozo, pamoja na ujenzi wa kituo cha afya Ngonga kituo kinachojengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya halmashauri.
Kituo cha Afya itunge umaliziaji wa ujenzi wa kituo hiki unaendelea.
Akizungumza kwa niaba ya wanakamati wenzake, Mwenyekiti wa kamati ya siasa Mkoa wa Mbeya, Mheshimiwa Jacob Mwakasole amesema;
Kamati ya siasa imefika wilayani Kyela kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo, hii ikiwa ni katika kutekekeza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi Chama kinachoisimamia serikali.
Aidha Mheshimiwa mwenyekiti alisema, kazi yao ni kushauri na kusema kama kunamapungufu yoyote katika kusimamia na kutekeleza miradi ya maendeleo yote inayoanzishwa kwa ajiri ya kutatua kero kwa wananchi.
Ujenzi wa Wodi ya mama na mtoto bado unaendelea.
Diwani wa kata ya Itunge Mheshimiwa Nickson Mwalukama, nae aliweza kutumia nafasi hiyo kuipongeza serikali kwa kuwaona wananchi wa kata ya Itunge hadi kuamua kuwaletea fedha zinazijenga kituo hicho cha afya. Pia alitoa pongezi kwa viongozi wa wilaya pamoja na wataalam wa wilaya ya Kyela, kwa kujitoa usiku na mchana katika kusimamia ujenzi wa kituo hicho cha afya.
Mwisho kamati ya siasa Mkoa wa mbeya ilikagua na kuridhishwa pia kuipokea miradi yote iliyokaguliwa katika wilaya ya Kyela na kutoa pongezi zao za dhati, kwa usimamizi mzuri wa miradi hiyo.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa