• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Maadhimisho Ya Siku Ya Wazee Duniani Yatumika kuwakumbusha Wazee Kufanya Mazoezi

Imewekwa Kwenye: October 1st, 2023

Haya yamezungumzwa  na Mgeni rasmi wa hafla ya maadhimisho ya siku ya wazee Duniani, Mhe. Katule G. Kingamkono ambae ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela, tarehe 01/10/2023.

Akitoa Hotuba yake katika viwanja vya KYECU vilivyopo kata ya Ipinda wilayani Kyela ,Mhe. Katule amesema, Ni muhimu wazee wakafanya mazoezi ili kulinda afya zao, kwa sababu mazoezi ni tiba tosha ya kuzuia magonjwa.

Amewataka wazee kufanya mazoezi ya kutembea kwa kuzunguka maeneo ya  nyumba zao au kufanya matembezi mafupi ili kuulinda mwili na  kuepukana na magonjwa ya uzeeni.

Pia amewakumbusha wazee kula vyakula vya asili zikiwemo mbogamboga na matunda ya asili kwani vyakula hivyo vina virutubisho vya kutosha.

Wazee wakiwa wamejipanga tayari kwa mashindano ya kufukuza kuku

Mheshimiwa Katule ametoa shukrani kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka wazee na kuwapa huduma za afya Bure kwa kupitia dirisha maalumu la wazee katika vituo vya kutolea afya.

Amesema yale yote ambayo wanawaahidi wazee kutokana na risala yao, yatafanyiwa kazi, ikiwemo kulishawishi baraza la madiwani liweze kukubali kutenga bajeti ya kuwakatia Bima ya afya wazee wachache kwa kila mwaka ili kuwasaidia katika matibabu.

Pia ameitisha kikao cha wadau siku ya tarehe 02/10/2023 ili kujadiliana suala la kuwasaidia kuwapa Bima wazee wasiojiweza kiuchumi ikiwa ni muendelezo wa huduma ya kuwapa kadi za Bima za bure wazee, kama walivyotoa kadi za bima zaidi ya 70 bure kwa wazee tarehe 01/10/2023 ikiwa ni siku ya maadhimisho ya wazee duniani.

Aidha amewataka wataalam kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya imani potofu juu ya wazee, ikiwemo mzee kuhusishwa na ushirikina pale anapokuwa na macho mekundu.

"Bila wazee hata sisi tusingekuwa hapa, wazee hawa walifyatua matofali wakajenga shule wakishirikiana na serikali na ndo maana sisi leo tumesoma na tumefika hapa."

Awali Mganga Mkuu (W) Dr. Saumu Kumbisaga, amewashukuru viongozi wa baraza la wazee kwa kukubali kufanya maadhimisho ya siku ya wazee duniani, katika wilaya ya Kyela ili kuleta chachu kwa wazee wengine kutambua kuwa wazee wanatambulika katika wilaya.

Aidha amesema wilaya ya Kyela inawategemea wazee ili iweze kupiga hatua kimaendeleo.

Mwisho Mwenyekiti wa baraza la wazee  Kyela ndugu Emmanuel R. Mwakalobo ametoa salamu zake kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka wazee katika suala la Afya.

Pia amewapongeza wataalam kutoka Ustawi wa jamii Wilaya ya Kyela, kwa kuwa karibu na wazee na kutoa msaada kwa wakati pale wanapopatwa na matatizo ya kiafya.

Mwisho

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa