• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mamlaka Ya Mji Mdogo Kyela Yazidi Kupaa Katika Ukusanyaji Wa Mapato

Imewekwa Kwenye: September 25th, 2022

Mamlaka ya Mji mdogo wa Kyela imezidi kupaa kimapato kuanzia robo ya kuanzia julai 1 mwaka 2021 hadi kufikia mwezi juni 30/2022,  kwa kukusanya jumla ya shilingi 387,545, 723/= ikiwa ni sawa na asilimia 96 ya makisio ya bajeti ya mwaka 2021/2022 ya shilingi 402,173,000/= kiwango ambacho hakijawahi fikiwa tangu kuanzishwa kwa Mamlaka hiyo.

Akitoa taarifa katika Baraza la mwaka la Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela lililofanyika katika ukumbi wa Mamlaka hiyo tarehe 23/09/2022, Mwenyekiti wa Mamlaka Mheshimiwa Emmanuel K. Bongo amesema;

Mamlaka ya Mji Mdogo Wa Kyela umefanikiwa kuchangia 10,000,000/= katika ujenzi wa zahanati ya Ndandalo, kuchangia mchanga katika ujenzi wa kituo cha Afya cha Itunge kituo kilichojengwa kwa fedha za tozo, uchangiaji wa shilingi 38,754,572.30 kwa ajiri ya ukopeshaji wa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambayo ni sawa na asilimia 100 ya uchangiaji.

Aidha amesema, Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela imefanikiwa kujenga vibanda 10 vya biashara katika stendi kuu ya mabasi hapa Kyela mjini. Pia Mamlaka ya Mji mdogo Kyela imetenga fedha shilingi 68,000,000/=  kwa ajiri ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, amabapo shilingi 30,000,000/= zimetengwa kwa ajiri ya ukarabati wa stendi ya mabasi  hapa Kyela mjini, Shilingi 15,000,000/= zimetengwa kwaajili ya ukarabati wa choo cha stendi, shilingi 20,000,000/= zimetengwa kwa ajiri ya kukarabati soko la olofea na shilingi 3,000,000/= zimetengwa kwa ajiri ya kuchangia ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Mbugani, Uhuru na Nkuyu.

Pamoja na hayo Mheshimiwa Bongo ametoa shukrani zake za dhati kwa ushikiano mkubwa uliopo baina ya Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Ismail Mlawa, Mbunge wa jimbo la Kyela Mhe ally Mlaghila Jumbe, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Katule G. Kingamkono, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Ndg. Ezekiel H. Magehema

pamoja na wataalam wote bila kumsahau mtendaji Mkuu wa Mamlaka hiyo Ndugu Gerald Mlelwa kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuongeza mapato katika Mamlaka hiyo.

Mwisho Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela Ndugu Gerald Mlelwa amesema; mafanikio yote yanayoonekana katika Mamlaka ni mchanganyiko wa juhudi kubwa za ushirikiano zinazofanywa na viongozi waliopo katika wilaya ya Kyela lakini pia ushirikiano mkubwa uliopo baina ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela na Halmashauri ya wilaya ya Kyela.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BIDHAA FEKI ZILIZOINGIA KWA NJIA HARAMU ZATEKETEZWA KWA MOTO

    July 01, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa