• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Mkoa Wa Mbeya Aagiza Madiwani Kupewa Elimu Dhidi Ya Mfumo Mpya Wa Ukusanyaji Wamapato

Imewekwa Kwenye: June 13th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera ameziagiza halmashauri zote mkoani hapa kutoa elimu kwa madiwani kuhusiana na mfumo mpya wa ukusanyaji mapato (Tausi) ili kudhibiti upotevu wa mapato wa halmashauri.

Amesema kuwa elimu hiyo itasaidia madiwani kuona umuhimu wa raha ya kukusanya mapato na kuyatumia  ikiwa ni pamoja na kuthibiti upotevu wa fedha.

Mhe. Homera amesema hayo tarehe 12/06/2023, katika kikao cha baraza maalum la kupitia hoja za mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali wilayani Kyela, mkutano uliohusisha madiwani, wakuu wa idara  na watumishi wa halmashauri pamoja na kamati ya ulinzi na usalama.

“Huu mfumo wa tausi umeletwa kwenye halmashauri zote za mkoa wa Mbeya, sasa Ofisa mapato na uongozi wa halmashauri tengenezeni semina maalum kwa madiwani hata ya siku moja ili kuwaelimisha waheshimiwa madiwani mfumo mpya wa ukusanyaji wa mapato” amesema .

Hata hivyo Mhe. Homera ameeleza kuwa halmashauri  zote za mkoa wa mbeya zinatakiwa kuelimisha madiwani  kuhusu mfumo huo wa ukusanyaji mapato wa Tausi  wajue faida zake na umuhimu wake na namna ya kushirikiana na wakuu wa idara katika ukusanyaji mapato.

Aidha Homera alizungumzia suala la ukusanyaji mapato kwa wilaya ya Kyela imefanya vizuri kwani ilitakiwa kukusanya Zaidi ya Bil.4. mpaka Juni 9, 2023  mmeweza kukusanya Zaidi ya Bil 4  ambayo ni sawa na asilimia 99.72.

“Ndugu zangu wana Kyela pia naomba muache tabia ya kuiua Kyela kimapato naomba ziishe waheshimiwa madiwani kuna wengine hawaitakii mema Kyela kabisa , tusiwadanganye wananchi, si mmeona ufuta kule Songwe wameuza 3700 wakati uuzaji holela ulikuwa shilingi 500 tuache kudanganya na serikali imeshatoa maelekezo kwa mazao ambayo yapo kwenye stakabadhi ghalani kupitia ushirika, likiwemo zao la kokoa ambalo ndilo chanjo kikuu cha mapato wilayani Kyela “amesema .

Diwani viti maalum wilayani Kyela , Tumaini Mwakatika amesema chama cha mapinduzi ni tanuri ambalo linapika vizuri viongozi ambao wanafanya kazi vizuri  kwa weledi mkubwa uliotukuka .

“Wewe mkuu wetu wa mkoa umepikwa vizuri tuna taarifa zako hata huko ulikotoka kuwa ulikuwa kiongozi wa mfano  hivyo tunakishukuru chama cha mapinduzi  kwa  jitihada kubwa za kuwandaa viongozi wake kwa umakini mkubwa.

Awari Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa alipata fulsa ya kutembelea bweni la wasichana katika shule ya sekondari Kiwira Coal Mine, pamoja na kufanya mkutano wa hadhara ili kusikiliza kero za wananchi katika kata ya Busale kijiji cha Lema.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa