• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Mkoa Wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera Akagua Miradi Ya Maendeleo na Kufanya Mkutano Wa Hadhara Kyela

Imewekwa Kwenye: October 10th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Juma Zuberi Homera, leo tarehe 10/10/2023, amekagua miradi ya maendeleo ikiwemo mradi wa ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu 3 ya vyoo katika shule ya msingi Mababu, ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu 3 ya vyoo katika shule ya msingi Mapinduzi kata ya Makwale, skimu ya umwagiliaji Makwale na kisha kumaliza ziara yake kwa kufanya mkutano wa hadhara katika kata ya Ngonga ili kusikiliza kero za wananchi.

Akiongea na wananchi wa kata ya Ngonga Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela, kumalizia jengo la maabara ndani ya siku 60, jengo linalojengwa katika kituo cha afya Ngonga.

Kuhusiana na kero ya barabara katika kata ya Ngonga Mhe. Homera, amewataka wataalamu wa TARURA, kufanya tathimini na kujua gharama ya ulimaji wa barabara katika kata ya Ngonga na andiko hilo lifike Ofisini kwake, ili alifanyie kazi, ila amewataka wataalamu hao, kuto andika gharama kubwa za ujenzi ambazo zinaweza leta ugumu katika utekelezaji wake.

Pamoja na hayo katika suala la umeme, Mhe. Mkuu wa mkoa amelitaka shirika la umeme wilaya ya Kyela kuorodhesha vitongoji vyote vilivyopo katika kata ya Ngonga, ambavyo havina umeme, na ambavyo havimo katika mpango wa kupata umeme kwa mwaka huu, ili aweze kuviombea bajeti kwa Mhe. Rais kwa mwaka huu, na kuvikamilisha kwa huduma ya umeme, amesema, anaamini jambo hilo litatekelezeka.

Aidha amemtaka mkandarasi anaeshughulikia mradi wa usambazaji wa maji hadi kata ya Ngonga, kukamilisha mradi huo hadi ifikapo tarehe 30/12/2023, ili wananchi wa Ngonga waweze kupata maji safi na salama.

Kuhusiana na suala la changamoto ya masoko ya matikiti, amemuagiza afisa kilimo wa wilaya kufanya tathimini ya idadi ya matikiti yaliyozalishwa ndani ya wilaya, ili kuyatafutia masoko nje ya wilaya ya Kyela.

Katika suala la kilimo, Mhe. Homera amesema, mbolea zitapatikana katika kata kwa kupitia chama cha msingi na  amemtaka mtendaji wa kata kubandika bei za mbolea mbalimbali katika kata, ili kila mwananchi ajue aina na bei ya mbolea.

Pia Mhe. Mkuu wa mkoa amechangia shilingi milioni 1 katika ujenzi wa bweni katika shule ya sekondari Ngonga, shilingi laki 5 kwa walimu wanaojitolea na kufanya vizuri na shilingi laki 5 kwa watumishi wa Afya wanaofanya kazi kwa bidii.

Mwisho aliwahakikishia wananchi kwamba Serikali ipo macho na itaendelea kutatua changamoto zote za wananchi.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa