Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa akizindua zoezi la uwekaji wa vibao vya anwani za makazi katika nyumba, ofisi na barabara wilayani Kyela.
Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa, amewahamasisha wananchi wa wilaya ya Kyela kushiriki katika kujitengenezea vibao vya namba zao za anuani za makazi.
Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ameyazungumza hayo tarehe 07/05/2022, akiwa katika tukio la uwekaji wa kibao cha anwani ya makazi katika ofisi yake. Mheshimiwa Ismail Mlawa amefanya hivyo ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa zoezi la uwekaji wa vibao vya anwani za makazi katika nyumba na barabara hapa wilayani Kyela.
Mkuu wa wilaya ya Kyela akihamasisha wananchi uwekaji wa vibao vya anwani za makazi Kyela.
Aidha amewahamasisha wananchi kutengeneza vibao vya namba za nyumba zao, kwani vibao hivyo havihitaji gharama kubwa sana, ni kiasi kisichozidi shilingi elfu tatu( 3000 ) kwa kibao kimoja. Kwa upande wa taasisi, Mheshimiwa Mlawa ameziomba taasisi zote zilizopo hapa wilayani, kushiriki katika kuchangia utengenezaji wa vibao vya anwani za makazi katika barabara mbalimbali na katika ofisi zao, ili kuufanya mji wa Kyela kupendeza na kutambulika kwa anuani hizo za makazi.
Nae Mwenyekiti wa anwani za makazi wa wilaya ya Kyela, Ndugu Arnold Selestine Mzigo amesema, hadi sasa zoezi la utambulishaji wa majina ya barabara za mtaa pamoja na uandika wa namba katika makazi ya watu umekamilika.
Zoezi linaloendelea ni utoaji wa elimu wananchi wa wilaya ya Kyela, elimu inayohusu jinsi ya uandaaji na uwekaji wa vibao vya anwani za makazi katika barabara nyumba binafsi, pamoja na taasisi mbalimbali.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa