Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Mheshimiwa Katule G.Kingamkono akiwa anazungumza na watenda kazi ya anwani ya makazi.
Haya yamezungumzwa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kyela, Mhe. Katule G. Kingamkono alipokuwa akifunga mafunzo ya watenda kazi ya anwani ya makazi kwa kata za mamlaka ya Mji mdogo Kyela, tarehe 13/03/2022 ndani ya ukumbi mkubwa wa halmashauri ya wilaya ya Kyela.
Watenda Kazi ya anwani ya makazi wakiwa wanamsikiliza Mwenyekiti wa halmashauri, wakati wa kufunga mafunzo ya anwani za makazi kwa kata 14 za mamlaka ya mji mdogo Kyela.
Akifunga mafunzo hayo Mheshimiwa Katule amesema yupo tayari kutoa zawadi ambayo hakuitaja kwa kata itayokuwa ya kwanza kumaliza zoezi hili, ikiwa ni pamoja na mtenda kazi wa kwanza kumaliza kazi yake aliyopangiwa.
Aliongeza kwa kusema, anayafanya haya ili kuwatia moyo na kuongeza kasi ya kazi. Pamoja na hayo alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri, kumuondoa mtendakazi yeyote atakaeonekana kutoendana na kasi ya kazi tunayoitaka kama wilaya.
Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela ndugu Ezekiel Magehema alisema, kwa sasa tumeajiri watenda kazi 100, watakaofanya kazi katika kata 14 za mamlaka ya mji mdogo Kyela, na baadae wataajiriwa wengine 200 kwa ukamilishaji wa kazi kwa wilaya nzima.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa