• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TASAF Yatoa Elimu Ya Matumizi Bora Ya Fedha Kwa Walengwa-Claudia U. Kitta

Imewekwa Kwenye: March 30th, 2019

Haya yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe. Claudia U. Kitta alipokuwa akitoa ufafanuzi wa utekelezaji wa mfuko wa kusaidia kaya masikini (TASAF), hapa wilayani Kyela tarehe 27/03/2019.

Akitoa ufafanuzi huo amesema; watalaam kutoka Halmashauri ya wilaya ya Kyela hupita kutoa elimu ya matumizi bora ya fedha wanazozipata walengwa kwa kila dirisha la malipo linapofunguliwa. Hivyo walengwa wengi wanapewa elimu juu ya matumizi ya pesa ambayo inatolewa ili kuwasaidia wananchi wote waishio katika mazingara magumu. 

Aidha alisema, mfuko huu umesaidia sana katika kuongeza nguvu kazi hapa wilayani Kyela, kwani mfuko huu umewagusa hata wananchi ambao ni waathirika wa VVU, ambao walikuwa hawana uwezo wowote wa kujipatia chakula, na hivyo kufanya afya zao kuathirika zaidi. 

Pamoja na hayo walengwa wengi ambao ni waathirika wa VVU na wale wazima, kwa pamoja wameishukuru serikali ya awamu ya tano, kwa kuwasaidia kupata hiki kidogo ambacho kimewasaidia kupata chakula, na kuwa na afya njema inayowasaidia wao kufanya shughuli ndogondogo za kimaendeleo na kuinua kipato chao.

Aidha Mkuu wa wilaya ya Kyela, amekuwa akifanya ziara za kutembelea walengwa wote wanaonufaika na mfuko huu. Hata Kama kuna mazuri mengi  ambayo yamekuwa yakifanywa na mfuko huu, ila kwa upande wake, amegundua changamoto ya watendaji kuchelewa kufika katika eneo la malipo na kufanya malipo  kwa walengwa.

Amesema,  tatizo hili linaweza kusababisha usalama mdogo wa fedha za walengwa, Hivyo  kwa kupitia changamoto hii Mkuu wa wilaya ya Kyela, amewataka watendaji na wahusika wote wanashughulika na malipo haya kuwahi kufika eneo la malipo ili kuondoa changamoto ya usalama kwa wapokeaji wa fedha  hizo.

Aidha alitoa shukrani zake za dhati kwa serikali ya awamu ya tano, kwa kusaidia wananchi wake kupitia mfuko huu wa TASAF, kwani kuna baadhi ya wanufaika wameweza hata kuanzisha vikundi vya kukopeshana. 

Kikundi cha Mwamko, kinachopatikana kijiji cha Kilombero kata ya Mababu hapa wilayani Kyela, ni moja kati ya vikundi vilivyofanikiwa kuchanga fedha hadi kufikia kiwango cha zaidi ya shilingi 1,500,000/= wakiwa na wanachama 20 chini ya mwenyekiti wao Essah Ijande.

Wanasema; wametumia elimu iliyokuwa ikitolewa na watalaam kutoka Halmashauri ya wilaya ya Kyela, elimu iliyokuwa ikisisitiza swala la walengwa kuunda vikundi na kusaidiana ili kukuza mitaji yao.

Wanakikundi hawa kila walipopata fedha katika dirisha la malipo, waliweza kuchangia kiasi cha shilingi 1000/= kwa kila mjumbe, hivyo pesa hiyo iliwasaidia kununua vifaranga 100 vya kuku na kugawana, ambapo hadi sasa kila mjumbe anakuku wasiopungua 15.

Aidha fedha zilizobaki zimewasaidia kuanzisha shughuli za kilimo kwa kukodi mashamba mawili, ambayo wamepanda mpunga, wanaotegemea kuvuna gunia zaidi ya 18.

Kikundi hiki kimekuwa na malengo mengi na makubwa kwa baadae, mfano; wamepanga kununua mashine ya kusaga na kukoboa, kununua shamba lao la kudumu, kufungua akaunti benki pamoja na kupata usafiri wa baiskeli ya kikundi.

Mwisho pongezi nyingi zilitolewa na wanufaika kwa serikali yao inayowajali, kwani imeweza kuwaondoa katika umaskini uliyokuwa umekisili miongoni mwao, pia imepunguza maradhi kama utapyamulo katika jamii zao.

Mmoja wa wanakikundi cha Mwamko akiwa na baadhi ya kuku wake

Baadhi ya wajumbe wa kikundi cha Mwamko wakiwa katika picha ya pamoja. 



Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa