• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Walimu Watakiwa Kuinua Taaluma Nchini

Imewekwa Kwenye: January 26th, 2019

Haya yamezungumzwa na naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe.Tixon Tuliangine Nzunda, alipokuwa akiongea na Wakuu wa shule, Walimu wakuu, pamoja na waratibu elimu katika ukumbi wa shule ya sekondari Kyela Day, iliyopo wilayani Kyela tarehe 25/01/2019.

Aidha amewataka walimu kufanya kazi kwa juhudi na maarifa makubwa, ili kuleta mabadiliko yenye tija katika elimu yetu Tanzania. 

Pamoja na hayo Mhe. Tixon Mzunda alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela, Ndugu Lucy L. Mganga kwakutoa mchango mkubwa unaowezesha ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa wilayani hapa. 

Pongezi zilitolewa kwa wilaya ya Kyela pia, kwani imejitahidi katika kufaulisha wanafunzi wengi, amesema wilayani ya Kyela imepata daraja la asilimia 52 kitaifa, na kumekuwa na ongezeko la wanafunzi 3096 wanaokwenda kuanza kidato cha kwanza, ambapo idadi hii ni kubwa ukilinganisha na miaka mingine iliyopita.

Kutokana na idadi hii ya wanafunzi kuongezeka, amewataka wakuu wa idara kwenda kuweka kambi katika maeneo yote ambapo madarasa yanajengwa, ili kuhakikisha madarasa hayo yanakamilika kwa wakati, na wanfunzi wote wanajinga na kidato cha kwanza kwa masomo. 

Aidha Mhe.Toxin Nzunda, amewaambia wakuu wa shule kwamba, kwa sasa wameongezewa nguvu yakuweza kuwapandisha vyeo walimu wanaofanya kazi vizuri na kuleta matokeo yenye tija. Ikiwa ni sehemu ya kuwatia moyo walimu hao. 

Hata hivyo ametaja maeneo mbalimbali ambayo yatatumika katika kumpima mwalimu, ikiwemo uandaaji mzuri wa mfumo wa ujifunzaji na ufundidhaji darasani, idadi ya vipindi vilivyofundishwa kwa somo na kwa mwaka pamoja na kuangalia kiwango cha ufauru wa wanafunzi kwa somo husika. 

Pia amewataka walimu wa shule za msingi kuhakikisha wanafundisha vizuri KKK, ili kuepusha kuwapeleka wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kidato cha kwanza. 

Amesema, kwa asilimia 12 ya walimu wetu ni watoro kazini, asilimia 38 ya walimu hufika kazini na kusaini lakini hawaingii kufundisha. Hivyo amewataka Wakuu wa shule kusimamia nidhamu na uwajibikaji wa walimu. Endapo watashindwa wataondolewa katika madaraka na kupewa mwalimu mwingine kutoka shule hiyo. 

Kuimarisha uongozi bora na ubunifu, iwe ni siraha ya kuleta mabadiliko chanya, katika kuinua taaluma mashuleni. 

Inetolewa na:

Mkurugenzi Mtendaji 

Ofisi ya Habari na Mahusiano 

Kyela. 

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa