Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mheshimiwa Katule G. Kingamkono akikabidhi msaada wa sare za shule na viatu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Nduka.
Wanafunzi wa shule ya Msingi Nduka, iliyopo kata ya Ngana wilayani Kyela wamenunuliwa na kugawiwa sare za shule pamoja na viatu, ikiwa ni ombi la wanafunzi hao kwa Mheshimiwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kyela wakati alipofanya ziara katika shule hiyo takribani mwezi 1 uliopita. Sare na viatu hivyo vimegawiwa tarehe 05/02/2022 zoezi lililofanyika katika kata ya Ngana.
Akizungumza na wananchi hao Mheshimiwa Katule alisema, anapaswa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjalia na hata kufanikiwa kuwanunulia sale na viatu vya shule wanafunzi hao, na anafanya hivi ili kukisaidia kizazi cha Nduka kufanikiwa katika elimu."
Wawakiliashi wa wanafunzi wa shule ya msingi Nduka wakiwa wamepoke sare za shule na viatu.
"Msaada huu si wangu peke yangu bali ni msaada kutoka kwangu na wadau wengine wa maendeleo ikiwa ni pamoja na mawazo mazuri ya viongozi wote wa wilaya ya Kyela, ila kwa upande wangu nitakuwa pamoja na wanaNduka kwa miaka yangu yote ya uongozi wangu hata nikiwa nje ya uongozi" alisema.
Pia Mheshimiwa Mwenyekiti alimuagiza mtendaji wa kata kuhakikisha wanakijiji cha Nduka wanapata miche ya michikichi ambayo inagawiwa bure na Halmashauri kwa wakulima.
Akiongea kwa niaba ya wananchi diwani wa kata hiyo Mheshimiwa Kajala alisema, Tunashukuru Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kutimaza ahadi zako, uliahidi kuwaletea wanafunzi daftari na umeleta, uliahidi kuleta sare za wanafunzi pamoja na viatu na umeleta, usafiri kwa walimu pamoja na umeme haya yote umeyafanya na yanatekelezwa.Mwisho Mheshimiwa diwani aliwataka wananchi wa Nduka kutekeleza ushauri alioutoa Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kyela, ushauri uliowataka wanakijiji cha Nduka kuishi kwa pamoja ili kuanza kupata huduma za msingi kwa pamoja.
Nae kaka mkuu wa shule Brain Benson alisema anashukuru kwa niaba ya wanafunzi wenzake, kwa kupata sare za shule na kwa niaba aliahidi kuwa watasoma kwa bidii.
Wanafunzi wa shule ya msingi Nduka wakisubiri kukabidhiwa sare na viatu vya shule kutoka kwa mwenyekiti wa halmashauri ya wialaya ya Kyela.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa