• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Maendeleo na Ustawi wa Jamii

 IDARA YA MAENDLEO YA JAMII 

Shughuli zinazotekelezwa na idara ya maendeleo ya jammi kwa kuzingatia sheria na miongozo iliyopo.

Kuhamasisha jamii kwa kuamsha ari kushiriki shughuli za maendeleo katika jamii katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa kuchangia nguvu zao na kuchangia fedha kwa maendeleo yao.

Kuratibu masuala ya ukatili wa Kijinsia katika Wilaya, ikiwa ni pamoja na kuratibu Mpango wa kuzuia Ukatili kwa wanawake na Watoto MTAKUWWA katika ngazi ya Jamii.

Kuratibu masula ya vikundi katika Wilaya kwa kuvisajili na kusimamia uendeshaji wao na utatuzi wa migogoro inayojitokeza katika vikundi.

Kuratibu Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na Vijana Ili kuwezesha Kiuchumi makundi hayo maalumu katika jamii kwa kutoa mikopo Isiyo na riba Kwa vikundi vya Wanawake,Vijana na Watu Wenye Ulemavu kwa asilimia 10 ya mapato  yanayotengwa na Halmashauri.

Kuratibu Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs), kuhakikisha yanafanya kazi kwa kuzingatia sheria Na. 24/2002 ya uanzishwaji wa mashirika yasiyo ya Kiserikali.

Kuratibu Mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI katika jamii ili kupunguza maambukizi mapya na kuhakikisha waliopimwa wanadumia dawa za Kufubaza virusi vya UKIMWI hasa ukizingatia maambuzi ni asilimia 9.3 zaidi ya maambukizi ya Kitaifa ambayo ni asiimia 4.7

Kuratibu shughuli za TASAF kiwilaya kwa kuwezesha kaya masikini kuwapatia fedha kaya maskini iliyoko kwenye mpango.

Kuwezesha usajili wa Vizazi na Vifo kwa Watoto Chini ya Miaka 5 na watu wazima.

Kuhamasisha ujenzi wa nyumba bora katika Jamii ili kuboresha makazi bora katika jamii zetu.

Kusimamia masuala ya vijana katika jamii ili kujitambua na kutambua fursa zilizopo Wilayani na kuzitumia kujiletea maendeleo.

Kuratibu masuala ya Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF) ili jamii ijiunge na kupata matibabu kwa gharama nafuu.

Kutoa elimu ya Lishe katika jamii ili kupata jamii yenye afya bora inayoweza kuchangia maendeleo katika jamii na elimu hii husisitiza sana lishe bora kwa Watoto wadogo wanaokuwa na hasa chini ya miaka 5

CHANGAMOTO

Uhaba wa wataalam katika Wilaya ambao unapelekea baadhi ya kata kukosa watumishi.

UTATUZI WA CHANGAMOTO

 

Tunatumia watumishi wa ugani wa idara zingine waliopo ngazi ya Kata kusaidia baadhi ya majukumu ya idara, pia kila mwaka tunaweka kwenye bajeti.

  • 12.  IDARA YA ARDHI NA MALIASILI.

Halmashauri kupitia Idara ya Ardhi na Maliasili infanya kazi zifuatazo:-

  • Kuandaa Mipango ya matumizi ya ardhi ya miji na vijiji
  • Kupima viwanja na mashamba kwa ajili ya umilikishaji
  • Kuandaa hati miliki za ardhi kwa maeneo ya miji na vijiji
  • Kushughulikia uhamisho wa ardhi iliyomilikishwa
  • Kufanya udhamini wa mali
  • Kushughukia migogoro inahusu masuala ya ardhi
  • Kusimamia ulipaji pango la ardhi
  • Kutoa ushauri kuhusiana na masuala ya ardhi

Changamoto zinazotukabili katika idara ya Ardhi na Maliasili.

  • Kutokuwa na watumishi wa kutosha katika idara ya ardhi mfano. Mipango miji hatuna hata mtumishi mmoja, Uthamini hatuna hata mtumishi mmoja.
  • Kutokuwa na Kifaa cha kisasa cha R.T.K G.P.S   kwa ajili ya kupimia viwanja.
  • Kutokuwa na usafiri wa uhakika kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za kila siku wa idara ya ardhi.

13.  KITENGO CHA MANUNUZI

Kwa mujibu wa Muundo wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela (Organisation Structure) na Sheria ya Ununuzi ya Umma Na.7 ya Mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2013, Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi kina majukumu yake kama ifuatavyo:-

Kusimamia majukumu yote ya ununuzi na Uuzaji kwa njia ya zabuni mali za Halmashauri kwa kufuata sheria na kanuni za manunuzi

Kusaidia kazi zinazofanywa na bodi ya zabuni

Kutekeleza maagizo ya bodi ya zabuni

Kuandaa mpango wa ununuzi wa Halmashauri na kusimamia utekelezaji wake

Kusimamia utunzaji wa ghala na Nyaraka (kumbukumbu ya vitu vilivyomo ghalani

Kukagua na kuandaa mahitaji ya manunuzi ya Idara na Vitengo katika Halmashauri

Kuandaa nyaraka za zabuni

Kuandaa matangazo ya huduma ya zabuni mbalimbali

Kuandaa taarifa ya kila mwezi ya manunuzi ya Idara na Vitengo na kuiwasilisha katika bodi ya zabuni

Kuandaa mikataba iliyoidhinishwa kwa wazabuni

Kutunza na kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka za ununuzi na uuzaji wa mali za hamashauri;

Kuandaa na kuhifadhi rejista ya mikataba ya wazabuni wanaoshinda zabuni;

Kuandaa taarifa za kila siku zinazofanyika katika stoo kuwezesha uhakiki wa mali na utunzaji katika stoo.

Kumshauri Mkurugenzi kuhusu manunuzi kwa kufuata kanuni na sheria.

Kushirikiana na Idara zingine katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri.

Kutekeleza maagizo mengineyo kutoka katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa