• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Huduma Za Elimu

IDARA YA ELIMU MSINGI

Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ina jumla ya shule za msingi 105. Kati ya hizo kuna shule za binafsi 2. Shughuli zote za idara zinasimamiwa kupitia vitengo 5 kama ifuatavyo:

  • Kitengo cha Taaluma.
  • Kitengo cha Vifaa na Takwimu.
  • Kitengo cha Elimu ya Watu Wazima.
  • Kitengo cha Elimu Maalum
  • Kitengo cha Utamaduni na Michezo.

2.1 Idadi ya wanafunzi

Idadi ya wanafunzi wa madarasa ya awali ni 6,448 wakiwemo wavulana 3,320 na wasichana 3,078 kwa shule 103 za Serikali na wanafunzi 81 kwa shule binafsi ambapo kati yao wavulana ni 49 na wasichana 32. Kati ya shule 103 za msingi za Serikali, shule moja ni ya mchepuo wa Kiingereza inayoitwa Nyasa English Medium Primary School.

Idadi ya wanafunzi wa darasa la I – VII ni 48789 ambapo kati yao wavulana ni 24596 na wasichana ni 24193 kwa shule za serikali na wanafunzi 375 wa shule binafsi ambapo kati yao wavulana ni 163 na wasichana ni 212.

Aidha, jumla ya wanafunzi wote kuanzia awali hadi darasa la VII ni 55,237 ambapo wavulana ni 27,966 na wasichana ni 27,271 kwa shule za Serikali.

Hali ya walimu wa shule za msingi hadi 30 Desemba, 2020 ni 896 ambapo wanaume ni 446 na wanawake ni 450. Uwiano wa mwalimu kwa wanafunzi ni 1:62. Hata hivyo Serikali imeajiri walimu 19 katika Halmashauri yetu ambapo wengine wanaendelea kuripoti.

2.2 Watoto wenye mahitaji maalumu

Halmashauri ina shule 2 zenye vitengo vya watoto wenye mahitaji maalum ambavyo ni shule ya msingi Kyela na Mwenge. Vitengo hivi vina jumla ya wanafunzi 68. Pia kuna kitengo cha wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule ya sekondari Kyela chenye wanafunzi 12. Aidha, Halmashauri ina mpango wa kuanzisha vitengo 2 katika shule za msingi Sama na Matema kwa ajili ya watoto wasioona na wenye matatizo ya akili.

Pia kuna vituo vya elimu ya watu wazima vyenye jumla ya wanafunzi 94 na vituo vya MEMKWA 12 vyenye jumla ya wanafunzi 144.

2.3 Hali ya ufaulu wa wanafunzi wa darasa la VII kuanzia 2015 – 2019

Hali ya ufaulu wa wanafunzi wa darasa la VII imekuwa ikipanda kutoka mwaka 2015 hadi 2019 kama jedwali linavyoonesha hapa chini;

 
Mwaka
Waliofanya
Waliofaulu
% ya Ufaulu
waliochaguliwa
wav
Was
jml
wav
was
jml
wav
was
jml
2015
3299
3570
6869
2115
1889
4004
58.29
2115
1889
4004
2016
3510
3781
7291
2048
2313
4361
59.82
2048
2313
4361
2017
3624
3714
7338
2418
2210
4628
63.07
2418
2210
4628
2018
3422
3509
6931
2654
2619
5273
76.08
2654
2619
5273
2019
2888
3109
5997
2529
2660
5189
86.51
2529
2660
5189

Aidha, kutoka mwaka 2006 hadi mwaka 2019 wanafunzi wote waliofaulu walijiunga na kidato cha kwanza.

2.4 Hali halisi ya miundombinu na samani

Na.
Miundombinu
Mahitaji
Iliyopo
Upungufu
% ya upungufu
1
Madarasa
1359
849
510
37
2
Nyumba za walimu
1359
191
1168
86
3
Matundu ya vyoo
2358
1364
994
42
4
Madawati
16626
17582
1338
8

2.5 Changamoto zinazoikabili idara

  • Upungufu wa walimu 427 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu1,323. Kwa sasa kuna walimu 896 wa shule za msingi.
  • Upungufu wa miundombinu ya vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, matundu ya vyoo vya wanafunzi na walimu, madawati, meza na viti unaotokana na ufinyu wa bajeti.
  • Wanafunzi kukosa chakula cha mchana shuleni
  • IDARA YA USAFI NA MAZINGIRA.

Idara ya usafi wa mazingira inatekeleza majukumu yafuatayo:-

  • Kusimamia kampeni ya usafi ya jumamosi mwisho wa mwezi.
  • Uzoaji taka ngumu maeneo ya Njisi, Ipinda, Boda na Ngekye.
  • Kutoa elimu ya usafi wa Mazingira na ujenzi wa vyoo bora na kufanya ukaguzi katika kaya.
  • Kutoa elimu ya usafi wa maingira katika majengo yote ya biashara na kufanya ukaguzi katika Hoteli, nyumba za kulala wageni, migahawa, taasisi za Umma na binafsi.
  • Kutoa elimu ya usafi wa mazingira katika maeneo ya mji na vijijini.
  • Kutengeneza viunga vya bustani (Land scapping)

CHANGAMOTO.

  • Kwa sasa tunagari mbili, ambazo zinatumika kuzoa taka ngumu. Ni magari ya zamani ambayo huaribika mara kwa mara mpaka sasa gari moja limeharibika hivyo kupelekea uzoaji taka kukwama na takataka kurundikana maeneo ya vizimba.
  • Katika mji wa Ipinda hakuna mahali pa kutupia takataka (Dampo) na kuna vizimba viwili na vinahitajiwa vizimba 3.
  • Mifereji hapa mjini katika barabara nyingi havijajengewa ili kurahisisha usafirishaji wa maji ya mvua (storm water) na badala yake mifereji imeziba wakati wa mvua nyingi.
  • Boda eneo la kijiji cha Kilasilo, Halmashauri ilinunua eneo la kutupia takataka (Dampo) bado mpaka sasa halitumiki. Eneo hili lingesaidia kama lingetengenezwa na kuanza kufanya kazi kutokana na mji wa Boda unavyokua.
  • Uhaba wa watumishi, kuna watumishi 3, mahitaji ni watumishi 30.
  • Ofisi ya Idara ya Usafi wa Mazingira ipo lakini ni mbovu nan i hatari kwa watumiaji.
  • Pia hakuna hakuna gari la taka maji (liquid waste truck emptier)
  •  IDARA YA ELIMU SEKONDARI

Idara ya Elimu ya Sekondari ina shule 28 zikiwemo shule 22 za serikali na shule 6 za binafsi. Idara ina jumla wanafunzi 15580 kwa shule za serikali na jumla ya walimu 678.

Idara ya Elimu Sekondari inayo jumla ya watumishi sita wa makao makuu ya Halmashauri ambao ni Afisa Elimu Sekondari, Afisa Elimu vifaa na Takwimu, Afisa elimu Taaluma Sekondari, Mtunza kumbukumbu za ofisi, Dereva na Mhudumu wa Ofisi.

Idara inatekeleza majukumu yafuatayo;

Kusimamia sera na miongozo inayotolewa na Serikali kuhusu elimu ya sekondari ndani ya wilaya.

Kusimamia, kuratibu na kufuatilia shughuli za ujenzi wa miundombinu katika shule za sekondari kama vile nyumba za walimu, madarasa, majengo ya utawala, maabara, makitaba na vyoo.

Kusimamia na kuratibu shughuli zote za ukusanyaji, uchambuzi na kutafsiri takwimu za Idara ya elimu sekondari na kuwasilisha sehemu husika.

Kusimamia na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata taaluma kwa kiwango kilicho bora kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya mwaka 1995 na 20014.

Kusimamia na kuhakikisha nidhamu ya wanafunzi, walimu na watumishi wasio walimu inadumishwa shuleni.

Kuandaa mpango na maksio ya bajeti ya idara ya Elimu ya Elimu Sekondari kila mwaka.

4.1 MIUNDOMBINU

MADARASA
VYOO
NYUMBA ZA WALIMU
Mahitaji 
Yaliyopo
Upungufu
Mahitaji 
Yaliyopo
Upungufu
Mahitaji 
Yaliyopo
Upungufu
417
393
33
607
362
230
622
51
571

Baadhi ya shule zimefika ukomo wa kuongeza madarasa kwa kuwa zimekuwa na idadi kubwa ya wanafunzi. Ufumbuzi ni kujenga shule mpya katika maeneo ambayo shule zake zimejaa mfano Kyela mjini idadi kubwa ya wanafunzi wanahitimu kila mwaka na kuwapeleka katika kata za pembezoni.

Kwa kuzingatia hilo idara imeandika andiko juu ya ujenzi wa zaidi ya vyumba 87 katika shule zilizopo na ujenzi wa shule mbili(2) mpya unaendelea katika kata za Busale na Njisi. Aidha, Ujenzi katika kata ya Busale unaendelea vizuri wakati kwa kata ya Njisi kasi sio nzuri.

Mpango mwengine ni ujenzi wa shule za Hosteli kwa ajili ya wasichana,  kwa kuanzia tulitenga shule ya Nyasa kwa kupeleka wanafunzi waliofaulu vizuri zaidi katika ngazi ya wilaya, tumepeleka wanafunzi kwa miaka 2 lakini kwa mwaka huu tumeshindwa kutokana na kukosekana kwa bweni.

Uhitaji wa huduma hii ni mkubwa kwani wazazi wengi wilayani Kyela wamekuwa wanahangaika kupeleka watoto katika wilaya za jirani kwenye hosteli.

4.2 UFAULU 

Ufaulu wa wanafunzi kwa ngazi ya Halmashauri umekuwa ukiongezaka ingawa tukilinganisha na Halmashauri zingine bado tunahitaji kuongeza nguvu zaidi.

 

Ufaulu Kidato cha Nne

Mwaka 2017
Mwaka 2018
Mwaka 2019
Waliofanya 
Waliofaulu
Asilimia
Waliofanya 
Waliofaulu
Asilimia
Waliofanya 
Waliofaulu
Asilimia
1956
1515
77.5
2088
1647
78.9
2546
2048
80.4

 

 

Ufaulu Kidato cha Sita

Mwaka 2017
Mwaka 2018
Mwaka 2019
Waliofanya 
Waliofaulu
Asilimia
Waliofanya 
Waliofaulu
Asilimia
Waliofanya 
Waliofaulu
Asilimia
367
363
98.9
198
196
99.0
198
198
100

4.3 MIKAKATI

Ujenzi wa hosteli na kuzitumia

Uchangiaji wa chakula cha mchana ili watoto wapewe muda wa ziada

Makambi kwa wanafunzi wa madarasa ya mitihani

Aidha, mbinu hizi zimeonesha kutoa matunda kwani tuna shule za mfano ambazo zimeonesha matokeo haya.

 Matokeo ya mwaka 2019 shule yetu ya Masukila Sekondari imeingia katika Shule kumi bora kitaifa kwa kushika namba ya 5 ikiwa ni shule pekee kwa mkoa wa Mbeya kwa Shule za Serikali

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa