• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA KYELA, MHE. JOSEPHINE MANASE, AMEKABIDHI HUNDI YA MFANO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA SITA HAMSINI NA TATU LAKI SITA (653,600,000/=) KWA VIKUNDI 70 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

Imewekwa Kwenye: September 22nd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, amekabidhi hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi milioni mia sita hamsini na tatu laki sita (653,600,000/=) kwa vikundi 70 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Hafla hiyo imefanyika tarehe 22 Septemba 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela.

Akizungumza wakati wa makabidhiano, Mhe. Manase alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuleta mkopo wa 10% wenye tija kwa wananchi. Amesema mkopo huo ni chachu ya maendeleo kwani unawawezesha wananchi kujipatia mitaji ya kukuza kipato na kujikwamua kiuchumi.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kyela kwa kusimamia ipasavyo fedha zinazotolewa kwa ajili ya mikopo hiyo. Vilevile, aliwataka wanufaika wote waliokidhi vigezo kuzingatia mafunzo waliyopatiwa na wataalamu ili kuepuka changamoto wakati wa urejeshaji wa mikopo.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndg. Keneth Nzilano aliwataka wanufaika kuwa mabalozi wazuri wa mikopo hiyo ya 10% inayotolewa na Halmashauri. Alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila mnufaika kufanya shughuli zao kwa weledi na kuhakikisha marejesho yanakamilika kwa wakati ili na wengine wapate nafasi ya kunufaika.

Hatahivyo Wanufaika wa mikopo hiyo walito shukrani zao dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela. Walisema mkopo huo umethibitisha dhamira ya serikali ya kuwakumbuka wananchi wote bila kuacha makundi maalumu ambayo mara nyingi yamekuwa yakikosa fursa za kiuchumi.

Vilevile waliongeza kuwa mikopo hiyo itawawezesha kuanzisha miradi mipya, kuboresha biashara zao zilizopo na hatimaye kukuza vipato vyao. Waliahidi kutumia mkopo kwa nidhamu na kuhakikisha marejesho yanafanyika kwa wakati .

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MILIONI 570 ZATOLEWA KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE PAMOJA NA WATU WENYE ULEMAVU

    January 07, 2026
  • MKURUGENZI MTENDAJI KYELA ADV. FLORAH A. LUHALA AWATAKA WATUMISHI WAPYA 50 KULINDA NIDHAMU YA KAZI NA KUHUDUMIA WANANCHI

    December 05, 2025
  • THOBIAS JOSEPH MWAMKONDA APITA KWA KISHINDO KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KYELA

    December 02, 2025
  • DC KYELA AONGOZA KIKAO KAZI NA WATENDAJI WA KATA, WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI

    November 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa