• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI MTENDAJI KYELA ADV. FLORAH A. LUHALA AWATAKA WATUMISHI WAPYA 50 KULINDA NIDHAMU YA KAZI NA KUHUDUMIA WANANCHI

Imewekwa Kwenye: December 5th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Adv. Florah A. Luhala, ametoa mafunzo maalum kwa watumishi wapya wa ajira mpya kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 05 Desemba 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri, ambapo watumishi hao walifundishwa masuala mbalimbali ikiwemo misingi ya utumishi wa umma, haki na wajibu wa mtumishi, misingi ya kisheria katika kusimamia haki za watumishi, pamoja na miongozo na sera zinazopaswa kuzingatiwa katika utendaji wa kazi serikalini.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Adv. Florah A. Luhala aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na ufanisi, huku wakizingatia maadili ya utumishi wa umma ikiwa ni pamoja na utunzaji wa siri za serikali na taarifa za wateja wanaowahudumia katika vituo vyao vya kazi.

Aidha, aliwakumbusha kuonyesha heshima kwa viongozi, kuwahi kazini, na kufuata waraka wa mavazi unaoongoza watumishi wa umma, akibainisha kuwa hayo ni mambo muhimu katika kuimarisha taswira ya utumishi wa umma na kuhakikisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Adv. Luhala alisisitiza pia umuhimu wa kutii sheria, kanuni na taratibu zote za kiutumishi, akionya kuwa kitendo cha kwenda kinyume na miongozo hiyo kinaweza kusababisha kuchukuliwa kwa hatua za kinidhamu ikiwemo kusimamishwa kazi au kufukuzwa kulingana na makosa yatakayobainika.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI KYELA ADV. FLORAH A. LUHALA AWATAKA WATUMISHI WAPYA 50 KULINDA NIDHAMU YA KAZI NA KUHUDUMIA WANANCHI

    December 05, 2025
  • THOBIAS JOSEPH MWAMKONDA APITA KWA KISHINDO KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KYELA

    December 02, 2025
  • DC KYELA AONGOZA KIKAO KAZI NA WATENDAJI WA KATA, WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI

    November 28, 2025
  • KYELA YAADHIMISHA SIKU YA UKIMWI DUNIANI

    November 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa