• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Livestock Services

IDARA YA MIFUGO NA UVUVI

Idara ya Mifugo na Uvuvi inatekeleza majukumu yake kwa wafugaji na wavuvi kama inavyoonesha hapa chini:-

Kufanya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo kwa wafugaji katika kata zote za Halmashauri.

Kukagua nyama na usafi wa machinjio mara kwa mara.

Kutibu magonjwa ya mifugo na kushauri wafugaji jinsi ya kukinga mifugo dhidi ya magonjwa.

Kutembelea wafugaji mara kwa mara na kuwapa ushauri fasaha wa kitaalam.

Kukusanya takwimu zote za maendeleo ya mifugo katika eneo la Halmashauri.

Kufanya uhamilishaji (Artificial Insemination) na uzalishaji (breeding) wa mifugo kwa jumla.

Kushauri wafugaji umuhimu wa kupunguza mifugo yao kulingana na maeneo/malisho.

Kutoa taarifa za milipuko ya magonjwa na viumbe waharibifu.

Kuandaa ratiba cha chanjo na mipango ya uchanjaji.

Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wakala wa pembejeo muhimu za mifugo.

Kuwa kiungo kati ya vikundi vya wafugaji na watafiti.

Kukagua na kuidhinisha vibali vya usafirishaji wa mifugo.

 Kuendeleza uvunaji endelevu wa samaki na viumbe wengine wa baharini, maziwa, mito, mabwawa na malambo

Kutoa ushauri wa kitaalam kuhusu uvuvi bora, utengenezaji na uhifadhi bora wa samaki na mazao ya uvuvi, biashara na masoko ya samaki pamoja na ufugaji wa samaki na viumbe wengine wa majini

Kutoa leseni za uvuvi na kuendesha mafunzo ya taaluma ya uvuvi.

Kusimamia na kutekeleza sheria za uvuvi (kwa mfano kuzuia uvuvi haramu).

Kuratibu shughuli za utafiti wa uvuvi.

Kutoa ushauri na mafunzo kwa wananchi juu ya uendelezaji na matumizi endelevu ya rasilimali ya uvuvi.

Kukagua ubora wa samaki na mazao ya uvuvi na kuweka viwango vya kitaifa

  • CHANGAMOTO

CHANGAMOTO/MAHITAJI
UTATUZI /SULUHISHO
1.
Ukosefu wa vitendea kazi kwa maafisa ugani (pikipiki, extension kits, life jackets)
Kupatikana kwa vitendea kazi hivi kwa kutenga fedha katika bajeti ya Halmashauri
2.
Kukithiri kwa uvuvi haramu
Kupatikana kwa boti ya doria kuthibiti uvuvi haramu
3.
Kutokuwepo kwa machinjio ya kisasa ya kuchinjia ng’ombe
Ili kuongeza mnyororo wa thamani kunatakiwa kupatikana kwa machinjio ya kisasa kupitia wadau mbalimbali, Halmashauri, Serikali kuu na wafadhili
4
Wavuvi kutumia zana duni kuvulia hivyo uvuvi kutoleta tija kwa wavuvi na uchumi
Kuwawezesha wavuvi kupata zana bora (boti na Injini). Wavuvi wanaweza kukopeshwa au Halmashauri kununua boti na injini na kuwakodisha wavuvi na kuwa chanzo cha mapato kwa Halmashauri na kuchangia pato la Taifa
5
Kutokuwepo kwa bwawa la kuzalishia vifaranga bora vya samaki (hatchery pond)
Kupatikana kwa bwawa la kuzalishia samaki kwani ufugaji wa samaki unakuwa kwa kasi lakini wafugaji wanshindwa kuzalisha kwa tija kutokana na kukosa vifaranga bora
6
Kuwepo kwa magonjwa ya mlipuko
Kuboresha afya ya wanyama kwa kuchanja wanyama dhidi ya magonjwa ya mlipuko (kimeta, kideri, ugonjwa wa ngozi, chambavu, kichaa cha mbwa)
7
Upungufu wa watumishi
Idara kupatiwa watumishi kuendana na ikama. Idara ina upungufu wa watumishi 73

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa