• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA KYELA APOKEA BOTI YA DORIA KWA AJILI YA ZIWA NYASA

Imewekwa Kwenye: August 23rd, 2025

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya, amepokea boti mpya ya doria iliyokabidhiwa na Jeshi la Polisi Tanzania leo, tarehe 23 Agosti 2025, katika Ziwa Nyasa, Kiwira Port.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Manase ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuongeza vifaa vya kuimarisha ulinzi na usalama katika Ziwa Nyasa.

Amesema boti hiyo itaongeza nguvu katika kuhakikisha usalama wa Ziwa Nyasa unasimamiwa ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na watu wachache wenye nia ovu. Aidha, amezitaka taasisi zote za ulinzi na usalama wilayani humo kuhakikisha boti hiyo inatunzwa na kutumika kwa ufanisi ili idumu kwa muda mrefu na kuleta manufaa kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamini Kuzaga, amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama wilayani Kyela, ikiwemo Jeshi la Uhamiaji na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kulitumia vyema boti hilo katika kuimarisha doria na kutokomeza uhalifu unaotokea kupitia Ziwa Nyasa, ikiwemo uvukaji haramu wa mipaka.

Ikumbukwe kuwa Ziwa Nyasa ni miongoni mwa maziwa makubwa nchini Tanzania, na kwa upande wa Wilaya ya Kyela linapakana na nchi ya Malawi. Uwepo wa boti hilo utarahisisha doria za mara kwa mara, kusaidia kudhibiti wahamiaji haramu na kulinda mipaka ya taifa kupitia ziwa hilo.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DC MANASE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI WA KADI ZA BIMA YA AFYA KWA WOTE KWA KAYA ZISIZO NA UWEZO (ZINAZOHUDUMIWA NA MPANGO WA TASAF)

    February 09, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI LAPOKEA KWA SHANGWE TAARIFA YA MHE. DC KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE NAKUAHIDI KWENDA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    February 09, 2026
  • MILIONI 570 ZATOLEWA KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE PAMOJA NA WATU WENYE ULEMAVU

    January 07, 2026
  • MKURUGENZI MTENDAJI KYELA ADV. FLORAH A. LUHALA AWATAKA WATUMISHI WAPYA 50 KULINDA NIDHAMU YA KAZI NA KUHUDUMIA WANANCHI

    December 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa