• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

55 Wapewa Mafunzo Ya Ujasiriamali Uongezaji Wa Thamani Mazao Ya Kilimo

Imewekwa Kwenye: May 6th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine K. Manase amehitimisha mafunzo ya uongezaji wa thamani mazao ya kilimo kwa wanawake wajasiriamali wilayani Kyela.

Akihitimisha mafunzo hayo ya siku 3 katika ukumbi wa Chuo cha "KPC" leo tarehe 6/05/2023, Mheshimiwa Manase amesema;

Anatoa shukrani zake za dhati kwa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kwa kutoa mafunzo kwa wanawake 55, ambapo anaamini mafunzo hayo ya uongezaji wa thamani kwa mazao ya kilimo yataleta matokeo chanya katika wilaya yetu ya Kyela na Taifa kwa ujumla.

Aidha Mhe. Mkuu wa wilaya, ametoa shukrani zake za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujenga mazingira mazuri ya ufanyaji wa biashara nchini, ikiwa ni pamoja na kufungua fulsa kwa wanawake wajasiriamali.

Amesema Mhe. Rais amefanya mapinduzi makubwa katika sekta za Utalii, Kilimo Afya, Elimu, Mahusiano kimataifa, miundombinu ya usafirishaji,  mfano mzuri ni uwepo wa meli zetu kubwa 2 za mizigo na 1 ya abiria katika ziwa Nyasa, Ujenzi wa barabara kutoka Ibanda hadi bandarini Kiwila na Itunge hapa  wilayani Kyela.

Pamoja na hayo Mheshimiwa Josephine K. Manase,  amewataka wanawake wote waliopata mafunzo haya, kuendelea kuwa wabunifu katika kutengeneza bidhaa zenye ubora utakaokidhi mahitaji ya hapa nchini na nje ya nchi.

" Ukimuelimisha mwanamke Umeielimisha jamii nzima, sasa kupitia sisi tuliopata mafunzo tukawe mfano wa kuigwa kwa wenzetu ambao hawajapata mafunzo haya" amesema Manase.

Pia Mheshimiwa Mkuu wa wilaya amesema mafunzo haya ni muhimu sana, kwani kilimo kimewekwa kuwa ni kipaumbele katika kujiletea maendeleo, na ndio maana tuna agenda 10/30, ambayo imeendelea kutekelezwa kwa utoaji wa ruzuku za pembejeo, kilimo cha umwagiliaji kuanzisha mashamba makubwa na mengine mengi.

Mwisho amesema wilaya ya Kyeka itaendelea kutoa ushirikiano kwa sekta binafsi ili kuhakikisha uwepo wa mazingira bora ya biashara kwa wajasiriamali wetu.

Kwa upande wake Afisa maendeleo ya Jamii ndugu Victor Kabuje, amewataka wanawake wote waliopata mafunzo haya kwa siku 3, kuyatumia mafunzo hayo katika kubadilisha maisha yao na atafurahi atakapoona mafunzo hayo yametoa matunda kwa wahitimu wote.

Kwa upande wake Afisa Mradi kutoka "TWCC" Bi. Cresensia Mbunda amesema lengo kubwa la kutoa mafunzo haya, ni kuwataka wanawake kwenda kuliteka soko la ndani na nje ya nchi na hasa katika Jumuiya ya Afrika ya Maendeleo ya Kusini mwa Africa ( SADC). Kwani mafunzo hayo yameshirikisha utoaji wa elimu ya biashara na fedha pia.

Lucia Mwaisumo mkazi wa Itunge kaskazini, ametoa shukrani zake za dhati kwa niaba ya wanafunzi wenzake na kusema, wanaishukuru "TWCC" kwa kuwapa mafunzo kwa siku 3 ambapo, wamejifunza mambo mengi hasa masuala ya ujasiriamali, ikiwemo Utengenezaji wa sabuni za miche, viungo kama pilau masala ambapo elimu hii inaenda kuwasaidia wao, katika kufanya kazi kwa vitendo na wanaamini kipato chao kinakwenda kuongezeka.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa