• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Acheni Uvuvi Haramu-Luaga Joelson Mpina

Imewekwa Kwenye: October 27th, 2019

Mhe. Luhaga Joelson Mpina (katika) akizungumza na wavuvi katika mwalo wa Kafyofyo Kyela. 

Haya yamezungumzwa na waziri wa wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Joelson Mpina, alipokuwa akizungumza na wavuvi katika mialo ya ziwa Nyasa hapa wilayani Kyela, tarehe 26/10/2019.

Akizungumza na wavuvi hao katika mwalo wa Kafyofyo uliopo katika kijiji cha njisi  kata ya Kajunjumele wilayani hapa, Mhe. Waziri amewataka wavuvi kuachana na mazoea ya uvuvi haramu, kwani serikali imejipanga kuanza msako mkali katika ziwa Nyasa dhidi ya wavivu wanaojishughulisha na uvuvi haramu. 

Pia amesema Serikali imejipanga kuanza doria hiyo siku ya tarehe 27/10/2019, kwani katika ziara yake katembea na watalam kutoka wizarani kwake, ambao watashughulikia swala hilo mara moja.

Aidha Mhe. Luhaga Joelson Mpina, ameahidi kuleta vifaranga vya samaki katika mabwawa yote ya samaki yaliyopo katika ziwa Nyasa, hii ni kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa samaki. 

Hata hivyo Mheshimiwa waziri, amewatoa wasiwasi wavuvi wote kwamba, haitapita wiki moja kuanzia sasa, wavuvi wote wataanza kupewa elimu ya uvuvi bora na salama, ili waweze kuvua kwa vikundi na baadae kuweza kupata mikopo kutoka serikalini. 

Akizungumza kwa niaba ya wavuvi  ndugu Andrew Mwaisemba amesema, ni kweli wavivu wengi walikuwa wakifanya uvuvi haramu katika ziwa Nyasa, na kusababisha ziwa kukosa samaki kabisa kwa sasa. Na alimwomba Mhe. Waziri kutatua changamoto za miundo mbinu mibovu, kuwawekea sehemu za kupumzika na kupewa mikopo. 

Mwisho Mhe. Waziri alipata fulsa ya kutembelea katika kata ya Matema na kuzungumza na wavuvi wa maeneo hayo pia. 


Waziri wa wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Joelson Mpina akiwasili katika mwalo wa Kafyofyo uliopo kata ya Kajunjumele wilayani Kyela. 

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa