• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Baraza La Madiwani Kyela La Wahakikishia Wananchi Utoaji Wa Huduma Bora Katika Hospitali ya Wilaya

Imewekwa Kwenye: March 2nd, 2023

Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya wilaya Kyela mkoani Mbeya, limempongeza na kumshukuru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, kwa kuboresha huduma za afya katika hospitali ya wilaya na hivyo kuwaondolea adha na kero kubwa ambayo walikuwa wanakumba nayo wananchi wilayani hapa.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Kyela, Katule G. Kingamkono, aliyasema hayo jana tarehe 01/03/2023, wakati akitoa taarifa kuhusu masuala ya afya wilayani Kyela ikiwa ni katika kikao cha baraza la madiwani kwa robo ya pili, Kikao kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa halmashauri uliopo Kyela mjini.

Mhe. Kingamkono alizitaja huduma zilizoboreshwa hospitalini hapo  ni pamoja na vipimo vya mashine ya X-Ray ambavyo vilikuwa ni adha na kero kubwa kwa wananchi wilaya ya Kyela.

"Nitumie nafasi hii kuwapa pole wananchi wote wa wilaya ya Kyela ndani na nje, ambao walipata adha na kero kubwa wakati walipokuwa wanaenda hospitali ya wilaya kupata huduma za kitabibu" alisema Kingamkono.

Aliongeza anapenda kuwatangazia rasmi wananchi  kwamba wameweka mashine ya kisasa ya X-Ray ambayo ni ya mfumo wa kompyuta tofauti na zile za zamani.

Mhe. Kingamkono alisema zamani wananchi walikuwa wanalazimika kusubiri wapigwe picha, Na kisha wasubirie waipepee picha ili ikauke ndipo iweze kusomwa taarifa zake lakini sasa hivi ni mfumo wa kompyuta ambao mgonjwa anaweza kujiangalia viungo vyake vyote vya ndani ya mwili wake.

Aidha Mwenyekiti halmashauri alisema, katika eneo la afya ya kinywa na meno,wamepata vifaa vya kisasa sasa hata huduma ya meno bandia na uzibaji wa meno yaliyotoboka sasa hivi wanao uwezo wa kusafishwa kisha kuzibwa meno yao yaliyotoboka.

Kwa upande wa chumba cha kutunzia miili ya marehemu, Kingamkono alisema wameweza kupata jokofu lenye uwezo wa kutunza miili sita kwa wakati mmoja na pia chumba kimeboreshwa na sasa kina hali bora zaidi.

"Vile vile, tumefanikiwa kununua mashine ya kisasa ya kufulia nguo ambayo kwa wakati mmoja inao uwezo wa kufua mashuka 50 ambayo itatusaidia sana katika masuala ya usafi katika hospitali yetu ya wilaya Kyela" alisema Kingamkono.

Kingamkono alilitaja eneo lingine lililoboreshwa ni chumba kwa ajili ya kufanyia mazoezi, kwa wale wanaokutwa na changamoto ya ugonjwa wa kupooza sehemu ya miili yao hivyo kwa sasa wanacho chumba maalum kwa ajili ya kufanyia mazoezi.

Matangazo

  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Nafasi Za Kazi Tangazo Jipya January 01, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

    March 21, 2023
  • Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Afanya Kikao Kazi Na Watumishi Ili Kusikiliza Kero Zao

    March 17, 2023
  • Kamati Ya Siasa Ya Mkoa Wa Mbeya Imetembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Wilayani Kyela

    March 11, 2023
  • Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

    March 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa