• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Baraza La Madiwani Lapitisha Rasimu Ya Bajeti Ya Shilingi Bilioni 41.9 Kyela

Imewekwa Kwenye: January 14th, 2022

Baraza la madiwani wa Halmashauri  ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya, limepitisha rasimu ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ikiwa na makisio ya shilingi bilioni 41.9 ikiwa na vipaumbele katika sekta ya afya, elimu  na miundombinu ya barabara.

Akizungumza katika baraza hilo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Katule Kingamkono alisema  rasimu hiyo ya bajeti yenye makisio ya fedha kiasi cha shilingi bilioni 41.9  kitasaidia  kutatua kero mbalimbali za wananchi  kwa kuhakikisha vituo vya Afya, ujenzi wa vyumba vya madarasa  na barabara vinakamilika.

Alisema miongoni mwa miradi inayopigiwa chapuo na bajeti hiyo ni ujenzi wa Kituo cha Afya cha Ngonga,  Njisi  na ukarabati wa miundombinu ya barabara na madaraja  kuzunguka wilaya hiyo.

“Tunawashukuru madiwani  kupitisha rasimu hii ya bajeti ambayo imesheheni masuala mbalimbali kwa maendeleo ya wilaya yetu ikiwamo matumizi ya ndani ambapo kiasi cha shilingi bilioni 4.6 kimetengwa aidha ruzuku za matumizi ya kawaida jumla ya bilioni 29, ruzuku za miradi ya maendeleo,”  alisema Kingamkono.

Aidha aliwaomba wananchi kuendelea kuiunga mkono serikali katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo   na kuwa waaminifu katika ulipaji wa kodi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Ezekiel Magehema wilaya hiyo inamshukuru Rais  wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fedha nyingi kukamilisha miradi mbalimbali ikiwamo ujenzi wa Kituo cha Afya cha Itunge na ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Aliongeza kuwa bajeti hiyo inakwenda kutimiza mahitaji ya wananchi kwa kujengewa vituo vya afya, zahanati na uboreshaji wa  elimu  kwa kuhakikisha  mazingira ya kujifunzia na kufundishia yanaboreshwa  huku wakizingatia mpango wa maendeleo kwa miaka mitano kitaifa na kimkoa sambamba na ukusanyaji wa mapato alisema Magehema.

Aidha aliongeza kuwa Wilaya hiyo imejipanga vyema kukusanya mapato   na kuvuka lengo la mwaka jana ambapo walikusanya asilimia 104 mwaka  2021/2022 na kwa hadi sasa wamefanikiwa kukusanya asilimia 53 na lengo ni kukusanya zaidi ya asilimia 100.

Alibainisha mgawanyo wa  fedha za ruzuku kutoka serikali kuu kuwa ni Elimu ya Msingi kimetengwa kiasi cha shilingi milioni 631. Elimu sekondari 605,  ardhi na maliasili milioni tatu.

Baadhi ya madiwani akiwamo wa viti maalum, Tumain Mwakatika alisema bajeti hiyo imegusia asilimia 10 ya wanawake na vijana na kwamba kupitia  fedha hizo jitihada za wananchi kujikwamua na umasikini zitaongeza.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa