• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Baraza La Madiwani Limewafukuza Kazi Watumishi 9 Kyela

Imewekwa Kwenye: November 7th, 2022

Watumishi 9 wa Halmashauri ya wilaya Kyela, mkoani Mbeya wamefukuzwa kazi, baada ya kushindwa kurejesha fedha za makusanyo ya mapato,walizokuwa wamezikusanya lakini hawakuziingiza katika akaunti ya halmashauri kwa miaka mingi.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kufanyika kwa vikao vyote vya kisheria, na watumimishi  hao wote wamebainika kwa makosa ya wizi, wa kukusanya fedha za umma pasipo kuziingiza katika akaunti ya halmashauri ambalo ni kosa la kisheria.

Aidha Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Kyela, Mheshimiwa Katule Kingamkono, alitoa maamuzi hayo tarehe 05/11/2022 mara baada ya baraza la madiwani, lililokuwa likiendelea katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo kujigeuza kuwa kamati ili kuweza kufikia maamuzi kuhusu suala hilo la muda mrefu.

Mheshimiwa Kingamkono alisema pale mtumishi wa umma anapokwenda kinyume na majukumu yake ikiwa ni uwajibikaji, masuala ya wizi ama kutumia nafasi yake vibaya, basi baraza la madiwani pia limepewa mamlaka kwa kutumia taratibu, sheria na kanuni za utumishi kuwashughulikia watumishi kwa kufuata taratibu hizo.

Aliongeza kwa kusema maamuzi haya yamefanyika baada ya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Ndugu Ezekiel Magehema na wataalaam kufanya michakato yao, Na baraza kutoa maelekezo ya kufanyika kwa mchakato huo ndani ya siku tisini, ambazo zipo kwa mujibu wa sheria.

Alisema fedha hizo zilitakiwa kuleta maendeleo kwa wananchi wa Kyela, lakini wakawa wanasubiri siku za kisheria zifike, kwa hiyo wanapenda kutoa taarifa kwa umma, kwamba yale ambayo walimuagiza mkurugenzi sasa taratibu zimekamilika.

Mheshimiwa Kingamkono alisema, vikao vyote vya kisheria vimetumika kutoa maamuzi hayo, kwa hiyo anatoa taarifa kwamba wale wote ambao wamebainika kwa makosa ya wizi, wa kukusanya fedha za umma pasipo kuziingiza katika akaunti ya halmashauri lazima waondolewe kazini.

“Kwa hiyo leo baraza la madiwani kwa mamlaka lililopewa, kwa vifungu ambavyo vimeanishwa katika kanuni za serikali za mitaa, namna ya kuendesha kwa hiyo tunao watumishi tisa ambao tumewafuta kazi” Alisema Mhe. Kingamkono.

Aliongeza kwa kusema, wataendelea kuchukua hatua za kisheria, pasipo kumuonea mtu sababu hao wanaowafuta kazi, hakuna aliyeonewa na kuwa ni aibu sana leo yupo mwananchi asipotoa michango anachukuliwa hatua, wengine wanapelekwa mahakamani, wanalipa adhabu, kisha watumishi wengine wanazitumia pesa hizo kinyume na taratibu, Baraza la Waheshimiwa madiwani kamwe haliwezi kuendelea kucheka na watu, ambao wamekusanya fedha za umma, na kuzila wakati fedha hizo zingeenda kuchochea zaidi maendeleo ndani ya halmashauri ya wilaya ya Kyela.

Mwisho…….

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa