• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Baraza La Robo Ya 4 La Mamlaka Ya Mji Mdogo Kyela Lafanyika Mkurugenzi Apongezwa

Imewekwa Kwenye: August 22nd, 2024

Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela Mhe. Emmanuel K. Bongo ameongoza mkutano wa baraza la wenyeviti la robo ya 4 ya mwaka 2023/2024, katika ukumbi wa mikutano wa  Mamlaka ya Mji Mdogo tarehe 21/8/2024.

Mkutano huo umehudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya wilaya ya Kyela Bi.Florah A. Luhala, viongozi  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani, wataalamu kutoka ngazi ya mkoa na wilaya.

 Akijibu maswali ya papo kwa papo yaliyoulizwa na baadhi ya wajumbe ikiwemo suala la malamlaka ya mji mdogo wa Kyela kurasimishwa kua halmshauri ya mji Mhe.  Mwenyekiti amesema"

"Taratibu zote zinapangwa na Serikali na yenyewe ndio inaamua mamlaka kua halmshauri ya mji, hivyo utekelezaji upo kwani tunakidhi vigezo vya mamlaka yetu kua halmshauri ya mji tundelee kuvuta subira kusubiri taratibu za kiserikali.

Katika mkutano huo  Mhe. Mwenyekiti  amesema mamlaka imeendelea kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa mapato ndani ya robo ya nne hadi kufikia 82%, kuimarisha miradi ya maendeleo ikiwemo utoaji wa fedha kwa haraka kwa  ukarabati wa soko la olofea, ujenzi wa jengo la kupumzikia abiria  stendi kuu ya mabasi Kyela, uboreshaji wa miundombinu ya barabara kata ya Serengeti.

Aidha Mhe. Bongo amempongeza Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri ya wilaya ya Kyela Bi. Florah A. Luhala kwa ushirikiano mzuri baina ya Halamashauri na Mamlaka hata kupelekea ukamilishaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kyela.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Kyela Ndg.Gerald Mlelwa, amewaomba viongozi waliohudhuria  mkutano huo kuhamasisha wananchi waliopo katika maeneo yao, kujitokeza kwa wingi kupokea Mwenge wa Uhuru unaotarajia kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo tarehe 28/8/2024.

Sambamba na hilo Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg.Gervas Deus ameishukuru Mamlaka ya Mji Mdogo, kwa ushirikiano mzuri na Chama Cha Mapinduzi, pia amewaomba viongozi kuhamasisha wananchi, kujiandaa na uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mwezi wa 11 mwaka huu.

Awali  Meneja msaidizi huduma ya mlipa kodi mkoa wa Mbeya Ndg. Stephen Kauzen  ameipongeza Halmshauri ya wilaya ya Kyela, kwa ukusanyaji mzuri wa mapato kwa miaka 3 mfululizo, pia amewaomba viongozi kuhamasisha wananchi kuwa na "taxpayer" identification number (TIN NUMBER) zitakazowasaidia kufanya shughuli zao ikiwemo biashara bila usumbufu.

Vilevile Kauzen amemuagiza Afisa elimu wa mapato ngazi ya mkoa kuja kutoa elimu kwa wananchi wilaya ya Kyela, juu ya umuhimu wa ukusanyaji mapato.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe  Hospital ya wilaya ya Kyela, Dkt. Saumu Kumbisaga amewaomba wananchi kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa kipindupindu.

Ikiwemo kufanya usafi wa mazingira, pia ameongeza, kusema kuwa serikali inapambana kudhibiti ugonjwa huu kwani mpaka sasa wameweza kutoa kinga (vidonge vya kuua wadudu) katika shule 161, pamoja na kufunga biashara ya chakula kwa baadhi ya migahawa isiyokidhi vigezo.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KYELA COCOA GIRLS SECONDARY SCHOOL YALETA TUMAINI JIPYA KWA WATOTO WA KIKE KATA YA NKOKWA

    June 03, 2025
  • MAMLAKA YA MJI MDOGO YAKUSANYA MILIONI 400 KWA KIPINDI CHA ROBO YA TATU

    June 02, 2025
  • WAH. MADIWANI WAIACHA HALMASHAURI YA WILAYA YA KYELA MAHALI SALAMA WAKUSANYA BILLION 8.1 MPAKA ROBO YA TATU

    May 29, 2025
  • KAMATI YA FEDHA,UONGOZI NA MIPANGO MIJI YA MAMALAKA YA MJI MDOGO KYELA IMEFANYA ZIARA YA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA KUPUMZIKIA ABIRIA KATIKA STENDI KUU YA MABASI

    May 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa