• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Choo Cha Kisasa Chakabidhiwa Mamlaka Ya Mji Mdogo Kyela

Imewekwa Kwenye: February 1st, 2023

Uongozi wa Kata ya Mwanganyanga wilayani Kyela, umekabidhi choo cha kisasa kwa Mamlaka ya Mji mdogo wa Kyela, leo tarehe 01/02/2023, kilichokuwa kinakarabatiwa katika eneo la soko la wakulima lililopo eneo la Olofea hapa wilayani Kyela.

Makabidhiano hayo yamefanyika mara baada ya uongozi wa kata ya Mwanganyanga kwa kupitia kamati ya ukarabati wa choo hicho kujiridhisha na ukamilifu wa ukarabati huo kukamilika.

Akitoa taarifa kabla ya makabidhiano ya choo hicho, Mtendaji wa kata ya Mwanganyanga ndugu Mjemaso A. Mwambungu amesema,

Ukarabati wa choo hicho ulianza tarehe 25/11/2022 mara baada ya Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji mdogo ndugu, Gerald Mlelwa kutenga na kuingiza kiasi cha shilingi 20,000,000/= katika akaunti ya kata, na kuanza ukarabati kwa njia ya "force account", hadi kukamilika kwake.

Aidha makamau mwenyekiti wa Mamlaka ya mji Mdogo wa Kyela Mheshimiwa Michael Mwakibinga, ameridhishwa na ukarabati wa choo hicho na kukubali kukipokea kwa matumizi ya wananchi.

"Niwapongeza viongozi, kamati ya ujenzi pamoja na wananchi wote walijitolea katika ukarabati wa choo hichi bila malipo yoyote na hatimae kukamilisha ukarabati huu" amesema Mhe. Mwakibinga.

Pamoja na hayo Mhe. Mwakibinga ameahidi kukitunza choo hicho kwani ni chanzo kizuri cha Mapato kwa Mamlaka ya mji mdogo, lakini pia choo hicho ni msaada si kwa wafanyabiashara wa soko la wakulima tu bali kwa wananchi wote wa wilaya ya Kyela.

Hata hivyo diwani wa kata ya Mwanganyanga Mhe. Alex Mwinuka, alimaarufu kwa jina la  Bonge, ameiomba Mamlaka kuendelea kulipia umeme katika choo hicho ili kuendelea kupata huduma ya maji katika choo hicho, kwani huduma ya maji inapatikana kwa nishati ya umeme chooni hapo.

Lakini pia aliwasihi wananchi wote kuendelea kukitunza choo hicho ili kiweze kudumu kwa mda mrefu zaidi.

Miundombinu ya maji iliyopo katika choo cha kisasa kilichopo katika soko la wakulima Olofea hapa wilayani Kyela.

Bafu lililopo katika choo cha kisasa katika soko la wakulima Olofea hapa wilayani Kyela.

Mwisho.

Matangazo

  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Nafasi Za Kazi Tangazo Jipya January 01, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

    March 21, 2023
  • Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Afanya Kikao Kazi Na Watumishi Ili Kusikiliza Kero Zao

    March 17, 2023
  • Kamati Ya Siasa Ya Mkoa Wa Mbeya Imetembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Wilayani Kyela

    March 11, 2023
  • Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

    March 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa