• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Akemea Vikali Kukengeuka Kwa Maadili Katika Jamii

Imewekwa Kwenye: April 7th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine Keenja Manase amekemea vikali vitendo vibaya vinanavyoendelea kufanyika katika jamii yetu, hasa vitendo vya Ushoga, Ulawiti na Ukatili dhidi ya wanawake.

Mheshimiwa mkuu wa wilaya amekemea vitendo hivyo wakati akifungua mafunzo Elekezi, kwa wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela, mafunzo yaliyofanyika tarehe 06/04/2023, katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo.

"Viongozi Tuwe mstari wa Mbele katika kutoa taarifa kwenye vyombo husika punde tunapoona au kusikia, mwananchi yeyote anafanyiwa vitendo hivyo ili tuweze kujenga kizazi chenye misingi na maadili mema katika jamii" amesema Mhe. Josephine Manase.

Hata hivyo Mheshimiwa Mkuu wa wilaya, amewataka viongozi hao kuwa mstari wa mbele katika kusimamia maadili katika jamii, kwa kukemea vitendo vyote viovu vinavyofanyika kinyuma na mila zetu za kiafrika.

Aidha Mheshimiwa Manase ametoa pongezi nyingi kwa wajumbe wa baraza hilo, ambao wamekuwa wakichapa kazi nzuri za usimamizi wa shughuli za maendeleo, na kuhakikisha kwamba sisi sote hatuwezi kumwangusha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa jitihada zake anazotufanyia wana Kyela hasa katika kutuletea maendeleo.

Amesema kazi zote zinazofanywa na baraza hilo, zinaonekana na viongozi wanaziona, ameongeza kusema, viongozi wote hapa wilayani Kyela wataendelea kutoa ushirikiano kwa baraza hilo, kadri watakavyoweza ili kuleta maendeleo kwa wilaya yetu.

Pamoja na hayo, Mhe. Mkuu wa wilaya ametoa shukrani zake za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuikumbuka wilaya yetu ya Kyela, Na  kutuletea miradi mingi ya maendeleo ikiwemo miradi ya ujenzi wa zahati, vituo vya afya, shule na miradi mingine mingi.

"Tutaendelea kuipeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi, na tutaendelea kuupiga mwingi sababu tupo ndani ya Chama Cha Mapinduzi na tunatekeleza Ilani ya Chama chetu" amesema Mhe. Josephine Manase.

Kwa upande wa mikopo ya 10% inayotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Mheshimiwa Mkuu wa wilaya amewataka viongozi hao kwenda kutoa elimu juu ya urejeshaji wa mikopo kwa vikundi vyote, ambavyo vimenufaika na mikopo hiyo kwa wilaya ya Kyela.

"Naomba sana viongozi msiwapitishie mikopo vikundi vyote ambavyo vina wanachama wasiotoka katika eneo lako la kiutawala" amesema Mhe. Mkuu wa wilaya.

Awali, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela, Mheshimiwa Michael Mwakibinga alitoa pongezi kwa wajumbe hao, katika suala la kufanya kazi kwa jitihada kubwa ya kuwaletea maendeleo wananchi wa wilaya ya Kyela pamoja na ukusanyaji mzuri wa mapato.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa