• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Awataka TANESCO Kutoa Elimu Ya Matumizi Ya Simu Kuunganishwa Na Huduma Ya Umeme

Imewekwa Kwenye: May 16th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine Manase amelitaka shirika la umeme TANESCO Kyela kwenda kutoa elimu ya kutumia simu za mkononi, ili mteja mpya aweze kulipa na kupata huduma ya kuunganishwa na huduma ya umeme.

Amewataka wataalam wa TANESCO Kyela, hadi kufikia tarehe 18/05/2023 wawe wamefika katika kata ya Njisi kutoa elimu, Ikiwa ni utatuzi wa moja ya kero iliyowasilishwa na baadhi ya wananchi wa kata ya Njisi, katika mkutano wa hadhara uliofanyika tarehe 16/05/2023 hapa wilayani Kyela.

Aidha amesema tunamshukuru Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuiletea maendeleo ya wilaya, tunaona miradi ya maendeleo ikitekelezwa kila upande.

Kuhusiana na suala la umeme wa REA, Mhe. Josephine, amewaambia wanaNjisi kuwa kata ya Njisi ipo ndani ya Mamlaka ya mji mdogo ambapo, wananchi wote wanaoishi ndani ya mamlaka wanatakiwa kulipa shilingi 320,000/= ili kuunganishwa na huduma ya umeme.

Kwa huruma ya Mhe. Rais. Dkt Samia Suluhu Hassan, ameunda timu ya kufanya tathimini katika vitongoji ili kubaini maeneo yote ambayo yatafanyiwa tathimini na kujiridhisha kupeleka umeme wa REA. Hivyo wananchi wawe na subira mpango huo utakamilika kila mwananchi atapata umeme wa REA katika maeneo teule.

Mhe. Mkuu wa wilaya, amekili kwamba maji ni changamoto kwa wilaya ya Kyela, lakini  kuna miradi ya maji inayotekelezwa hadi sasa ingawa bado haijakamilika.

Kero ya baadhi ya wananchi kujichukulia sheria na kujenga nyumba katika mipaka ya barabara, Mhe. Mkuu wa wilaya amewataka wananchi wote wawe walinzi kwa wananchi wenzao, ambao wanajenga katika maeneo ya barabara na kutoa taarifa mapema pale inapobainika.

"Ninatoa onyo kwa  wenyeviti wa vitongoji wote, Kwa muda wote ambao nitakuwepo hapa, nisisikie mwenyekiti ameuza eneo bila kuwa na ushahidi wa kutosha, tutagombana".amesema Mhe. Josephine.

Mwisho amesema, Leo ni siku ya maadhimisho ya siku ya Familia duniani, amewakumbusha wazazi kuwalea watoto katika malezi bora, amesema tusipo walea watoto katika maadili mema, kizazi kijacho kitakuwa ni kizazi cha ajabu.

Aliendelea kusema jukumu la kulea watoto ni la Baba, Mama na jamii nzima, hivyo amewaomba wazazi kujenga familia zenye misingi bora. Pia amewataka kutoa taarifa wanapoona mtu yeyote anakwenda tofauti na maadili yetu.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela, ndugu Ezekiel H. Magehema amesema, Hatuna budi kumpongeta Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kwa kutuletea miradi mingi katika wilaya yetu, Na kuhusiana na suala la nyumba za watumishi amewaomba wananchi kuandaa maeneo kwani, nyumba za watumishi zitajengwa na zitajengwa kwa awamu.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa