• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC MANASE AWAHIMIZA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Imewekwa Kwenye: July 15th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe. Josphine Manase amefanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za Wananchi katika vijiji vya Masebe One na Bwato leo tarehe 15.07.2025, ambapo ametoa maelekezo na ushauri mbalimbali kwa maendeleo ya Vijiji vya Masebe one na Bwato Pamoja na Kyela kwa ujumla.

Akizungumza katika Ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kyela amewahimiza vijana kuchangamkia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, ili waweze kubuni biashara mbalimbali zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Aidha DC Manase amewahamasisha vijana kuendelea kujituma na kujiimarisha kimichezo kwa kujenga timu katika ngazi ya vijiji, ili baadaye zipatikane timu bora zitakazoiwakilisha Wilaya katika mashindano mbalimbali. Amesema kuwa viwanja vipo na fursa zipo, hivyo kinachotakiwa ni juhudi, nidhamu na mshikamano miongoni mwa vijana.

Mkuu wa Wilaya ya Kyela ameahidi kulifanyia kazi suala la kutokuwajibika kwa watoa huduma katika Kituo cha Afya cha Ipinda. Amewataka watoa huduma wote wa afya kuwajibika ipasavyo katika nafasi zao na kuacha mara moja tabia ya kuwakwamisha wananchi kupata huduma stahiki. Amesisitiza kuwa Serikali haivumilii uzembe au utovu wa maadili katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Adv.Florah A. Luhala akijibu kero Kuhusiana na kupanda na kushuka kwa bei ya zao la kakao, Mkurugenzi ameeleza kuwa zao hilo kwa sasa lipo katika mfumo rasmi wa TMX ambapo wanunuzi huongozwa na soko la dunia.

Pia amewashauri wakulima kutunza kakao vizuri na kuacha tabia ya kuuza kakao mbichi kwani inaharibu sifa ya kakao ya Kyela inayotambulika kimataifa.

Mkurugenzi amehimiza wazazi kuhakikisha kuwa watoto wote waliotimiza umri wa kuanza shule hawakai nyumbani kwa shughuli nyingine, bali waandikishwe na wahudhurie masomo kama inavyotakiwa kisheria na kwa manufaa ya maisha yao ya baadaye.

Mkurugenzi amewahimiza wananchi wote kushirikiana na Serikali katika kulinda heshima ya kakao ya Kyela na kuifanya kuendelea  kuwa bora duniani.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DC MANASE AWAHIMIZA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

    July 15, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AENDELEA NA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUZIPATIA UFUMBUZI KERO MBALIMBALI ZINAZOWAKABILI WANANCHI

    July 14, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA ISANGA WAPATA FARAJA KWA KUUNGWA MKONO NA MHE. DC MANASE KWA UANZISHWAJI WA UJENZI WA ZAHANATI

    July 12, 2025
  • TSH. MILLIONI TANO (5) KUTOKA MFUKO WA ZAO LA KAKAO KUSAIDIA UANZISHWAJI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA MSINGI KIJIJI CHA MPEGERE KATA YA MAKWALE

    July 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa