• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DED KYELA AWATAKA WASIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA KWENYE MIRADI

Imewekwa Kwenye: July 29th, 2025

Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela imefanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Kata ya Katumbasongwe, tarehe 29 Julai 2025.

Katika ziara hiyo, kamati ilitembelea miradi ya sekta ya afya, kilimo na elimu, ambayo inatekelezwa kwa ushirikiano wa Serikali Kuu, Halmashauri, wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Mojawapo ya miradi hiyo ni ujenzi wa Zahanati ya Itekenya Mpunguti, ambapo fedha zimetoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo michango ya wananchi  ni Shilingi milioni 27, na fedha kutoka Serikali Kuu ni Shilingi milioni 30. Hadi sasa mradi huo umefikia hatua ya upigaji ripu nje na ndani, na unatarajiwa kuboresha huduma za afya kwa wakazi wa eneo hilo.

Kamati pia ilikagua ujenzi wa nyumba ya Afisa Ugani, ambapo mradi umegharimu jumla ya shilingi milioni 50 zilitolewa kutoka vyanzo mbalimbali. Ikiwemo Wizara ya Kilimo ilichangia Shilingi milioni 40, lakini pia Halmashauri ya Wilaya ya Kyela kupitia Mapato ya ndani ilitoa shilingi milioni 9,364,000 huku wananchi wakichangia Shilingi 350,000.

Katika sekta ya elimu, kamati ilitembelea ujenzi wa bweni la wanafunzi katika Shule ya Sekondari Katumbasongwe. Ambapo kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela imetoa kiasi cha shilingi milioni 50 na ujenzi umefikia hatua ya upigaji ripu. Kukamilika kwa bweni hili kutasaidia kupunguza changamoto kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufuata masomo yao.

Aidha, kamati ilikagua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Isaki, ambapo mradi  unagharimu Tsh 125,000,000 mpaka kukamilika kwake mpaka sasa zaidi ya shilingi Milioni 70 kutoka vyanzo mbalimbali zimetolewa, Ikiwemo michango ya Wananchi walichangia shilingi Tsh.16,519,000 Halmashauri ya Wilaya ya Kyela imetoa shilingi milioni 13, Fedha kutoka Serikali Kuu ni shilingi milioni 30, Mamlaka ya Bandari shilingi milioni 5,940,000 Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata shilingi elfu 30, wadau wengine shilingi milioni 2,258,000 na Mfuko wa Mbunge shilingi milioni 2,500,000. Mradi huu unatarajiwa kuboresha huduma za afya kwa wakazi wa Kijiji cha Isaki kwa kuwapatia huduma ya haraka na ya karibu.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Adv. Florah A. Luhala, amewataka viongozi wa kata kuhakikisha kuwa fedha zinazotolewa na Serikali na wadau mbalimbali zinasimamiwa kikamilifu ili miradi ya maendeleo ikamilike kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MKUTANO WA MWAKA WA IDARA YA AFYA NA LISHE WAFANYIKA WILAYANI KYELA

    August 01, 2025
  • DED KYELA AWATAKA WASIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA KWENYE MIRADI

    July 29, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA KYELA Adv FLORAH A. LUHALA AONGOZA TIMU YA MENEJIMENT YA KAMATI YA ELIMU NA AFYA KUKAGUA MIRADI.

    July 28, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA ATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    July 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa