• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

HUNDI YA TSH 816,831,820 YATOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

Imewekwa Kwenye: February 11th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe.Josephene Manase amekabidhi mfano wa hundi ya mkopo wa 10% Tsh.  816,831,820.00 iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya Wanawake,Vijana na watu wenye Ulemavu katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri tarehe 11.2.2024.

Akikabidhi hundi hiyo Mhe. Mkuu  wa Wilaya ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwakumbuka wananchi wake kwa kutoa mkopo huo.

Mhe.Mkuu wa Wilaya amewapongeza wanufaika wa mkopo huo na kuwasihi kutumia vizuri fedha watakazopata ili waweze kujikwamua kiuchumi,kufanya shughuli za maendeleo ili waweze  kufikisha malengo yao.

Aidha Mkuu wa Wilaya amewaasa wanufaika hao kurejesha mkopo kwa wakati ili watu wengine waweze kunufaika,pia amewataka Wanufaika kuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao juu ya suala upatikanaji wa mkopo.

Pia Mhe.Manase amewaonya wale wote wanaotumia kigezo cha mkopo kutapeli watu, kuacha mara moja tabia hiyo kwani wakibainika hatua kali za kisheria zitachukiliwa dhidi yao.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Bi.Florah A. Luhala ameipongeza Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kufanya mchakato mzima tangu usajili wa vikundi na ufuatiliaji wa fedha hizo ili kuhakikisha zinawafikia walengwa.

Sambamba na hilo,Bi.Flora A.Luhala amesema mkopo huo ukawe chachu ya kubadilisha maisha kwa kufanya shughuli za maendeleo zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Wakizungumza kwa niaba baadhi ya wanufaika wa mkopo huo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea mkopo huo kwani utawasaidia kujiondoa kwenye mkopo wa kausha damu ambao umekua changamoto  miongoni mwa wananchi wengi.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO AONGOZA MCHAKATO WAKUMPATA MAKAMU MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO NA WENYEVITI WA KAMATI ZA KUDUMU

    October 01, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI ADV. FLORAH A. LUHALA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MAPATO YA HALMASHAURI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    September 30, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA, MHE. JOSEPHINE MANASE, AMEKABIDHI HUNDI YA MFANO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA SITA HAMSINI NA TATU LAKI SITA (653,600,000/=) KWA VIKUNDI 70 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    September 22, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AFUNGA MAONESHO YA KUSINI INTERNATIONAL TRADE FAIR AND FESTIVAL YA MWAKA 2025

    September 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa