• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Waheshimiwa Madiwani Kutoka Nchi Ya Malawi Wafanya Ziara Ya Siku Moja Wilayani Kyela Nchini Tanzania

Imewekwa Kwenye: June 4th, 2021

Waheshimiwa Madiwani 9 wakiongozana na maafisa 2, mwandishi wa habari 1, kutoka wilayani M’mbelwa mkoani Mzimba nchini Malawi, wamefanya ziara hapa nchini katika wilaya ya Kyela wakiwa na lengo la kujifunza shughuli zinazofanywa na kamati ya fedha ya waheshimiwa madiwani, mikakati inayofanywa na wilaya katika kukusanya mapato, shughuli zinazofanywa na baraza la madiwani, kazi zinazofanywa na waheshimiwa madiwani katika kuleta maendeleo ya nchi, Mahusiano baina ya Baraza la madiwani na ofisi ya Mkuu wa wilaya, pamoja na idara mbalimbali zinavyotoa huduma kwa wananchi.

Ziara hiyo imefanyika  tarehe 02/06/2021, ambapo wageni hao walipokelewa  na Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Mheshimiwa  Katule G. Kingamkono katika eneo la Boda Njisi na kisha kuwapeleka hadi katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kyela.

Akiongea na Mkuu wa wilaya ya Kyela, Kaimu Mkuu wa wilaya ya M’mbelwa  Nchini Malawi Mheshimiwa Steve Chima amesema, wameamua kufanya ziara katika Nchi ya Tanzania katika wilaya ya Kyela kwa lengo kubwa la kutambua ushirikiano uliopo baina ya nchi hizi mbili, ikiwa ni pamoja na kujifunza njia zinazotumika katika kukusanya mapato ya serikali.

Nae Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Claudia U. Ktta aliwapongeza wageni hao kwa kuona fahari kutembelea nchi yetu hususani katika wilaya ya Kyela. Alisema ziara hii, inaongeza mahusiano mazuri zaidi baina ya nchi zetu.

Aidha waheshimiwa madiwani kutoka nchi ya  Malawi walipata fulsa ya kufanya kikao kifupi na waheshimiwa madiwani kamati ya Fedha wa Tanzania katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kyela. Wakiendelea na kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela, ndugu Ezekiel Magehema kwa kupitia afisa utumishi wa wilaya, aliweza kutoa taarifa fupi ya shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na wataalam wakishirikiana na Waheshimiwa madiwani , ambapo taarifa hiyo iliibua majadara mzuri baina ya Waheshimiwa madiwani kutoka nchi ya Malawi na waheshimiwa madiwani wa hapa nchini Tanzania. Katika mjadara huo waheshimiwa madiwani kutoka Nchi ya Malawi waliweza kufahamu jinsi kikosi kazi cha ukusanyaji wa mapato(Task Force) kinaweza kufanya kazi ya ukusanyaji wa mapato bila kuathiri au kudhurumu haki za wananchi.

Mwisho Mwenyekiti wa Baraza la madiwani Nchini Malawi Mhe.Wishart A. Malinga alitoa pongezi za dhati kwa ukarimu wa WaTanzania na aliwaomba Waheshimiwa madiwani wa wilaya ya Kyela kufanya ziara nchini Malawi ili nao wapate kujifunza mambo mbalimbali ya maendeleo katika nchi hiyo.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BIDHAA FEKI ZILIZOINGIA KWA NJIA HARAMU ZATEKETEZWA KWA MOTO

    July 01, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa