• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Katibu Tawala Mkoa Wa Mbeya Awataka Watumishi Wa Serikali Kufanya Kazi Kwa Bidii Na Kuheshimiana

Imewekwa Kwenye: November 24th, 2022

Katibu tawala wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Lodrick Lazaro Mpogoro, amefanya ziara katika wilaya ya Kyela na kupata fulsa ya kuongea na watumishi wa serikali ndani ya Ukumbi wa Halmashauri hapa wilayani Kyela, ziara hii imegusa masuala ya  kukumbushana taratibu, kanuni za kazi katika utumishi wa umma. Ziara hii imefanyika leo tarehe 24/11/2022.

Aidha Ndugu Mpogolo amesema, amekuja kujitambulisha lakini pia kuwaunganisha watumishi wote wanaofanya kazi wilayani na wale wanaofanya kazi Mkoani. Amewataka watumishi kufanya kazi kwa pamoja kwa kufuata kanuni na tarazibu za utumishi wa umma. Pia amewasihi watumishi wanaofanya kazi Mkoani kuwa karibu na wale wanaofanya kazi wilayani, kwani kwa kupitia umoja huu maendeleo yatapatikana kwa kasi zaidi ya hapa tulipo.

Amesema mafanikio yoyote yale ya kimaendeleo katika nchi yanatokana na wataalam kwa kutimiza majukumu yako, lakini kufanya kazi kwa kuheshimiana. "Mkuu wa Idara yeyote ambae atamdharau msaidizi wake huyo hatufai katika Mkoa wa Mbeya" alisema Ndugu Mpogolo.

Pamoja na hayo, Mheshimiwa Katibu tawala Mkoa amewapongezi wataalam wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela kwa kufanya kazi vizuri na kusimamia miradi ya maendeleo inayoshamiri katika wilaya ya Kyela.

Wakati huo huo ndugu Mpogolo, ameipongeza Halamashauri ya wilaya ya Kyela kwa ukusanyji mzuri wa mapato, maana hadi kufikia sasa Kyela ni Halmashauri ya 3 ikiongozwa na Halmashauri ya Chunya, Busokelo kwa ukusanyaji wa mapato.

Akimaliza kutoa ujumbe wake Ndugu Katibu tawala Mkoa wa Mbeya, amewaasa watumishi kuachana na ulevi wa pombe kwani kunywa hadi kupitiza viwango hupunguza ufanisi wa kazi kwa mtumishi yeyote.

Akitoa salama za shukrani Mganga Mkuu wa wilaya ya Kyela ndugu Mariam Ngwere amesema, sisi kama watumishi tumeyapokea yote tuliyoelekezwa na kiongozi wetu na tunaahidi kuyafanyia kazi.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DC MANASE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI WA KADI ZA BIMA YA AFYA KWA WOTE KWA KAYA ZISIZO NA UWEZO (ZINAZOHUDUMIWA NA MPANGO WA TASAF)

    February 09, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI LAPOKEA KWA SHANGWE TAARIFA YA MHE. DC KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE NAKUAHIDI KWENDA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    February 09, 2026
  • MILIONI 570 ZATOLEWA KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE PAMOJA NA WATU WENYE ULEMAVU

    January 07, 2026
  • MKURUGENZI MTENDAJI KYELA ADV. FLORAH A. LUHALA AWATAKA WATUMISHI WAPYA 50 KULINDA NIDHAMU YA KAZI NA KUHUDUMIA WANANCHI

    December 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa