• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kiasi Cha Shilingi Millioni 110 Kimetolewa Kwa Vikundi Vya Ujasiliamali Kyela.

Imewekwa Kwenye: April 14th, 2021

Kiasi hicho kimetolewa katika semina ambayo ilihudhuriwa na; Mwenyekiti wa halmashauri ya kyela, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya kyela, Afisa maendeleo jamii na viongozi wengine kutoka katika taasisi tofauti pamoja na wajasiliamali kutoka sehemu mbali mbali za wilaya ya kyela tarehe 13/4/2021 ndani ya ukumbi wa mamlaka ya mji mdogo wa kyela, kwaajili ya kuwaendeleza wajasiliamali wadogo wadogo wakiwemo wanawake, vijana na walemavu.

Akizungumza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya kyela ndugu, Ezekiel Magehema katika semina hiyo amesema kuwa, hii sio mgao wa fedha ambayo haitarejeshwa, fedha hii ni mkopo ndio maana tunalazimika kutoa mafunzo kila wakati na kuhakikisha kwamba mikopo inarejeshwa kwa wakati, lengo kubwa ni kuwataka wajasiliamali wakafanye yale yaliyo dhamiliwa kufanya, watengeneze faida na warudishe mtaji wakati huo shughuli zao zikiendelea.

Pia, ndugu mkurugenzi ameongeza kwa kusema, kuna vikundi vilifanya vizuri, na vingine vilifanya vizuri zaidi, hivyo basi kwa vikundi ambavyo vilifanya vizuri zaidi hatukusita kuongeza nguvu zaidi katika vikundi hivyo.

Aidha, mwenyekiti wa halmashauri ya kyela mhe.Kature Godfrey Kingamkono amesema kuwa, faida ya kulipa mapato na ushuru haya ndio matokeo yake, hizi pesa hazijatoka serikali kuu, zimekusanywa kwenye mikokoa, mawese na maeneo mengine yote. Hivyo watendaji wa kata na vijiji wanapokuja kuchukua ushuru tusijenge uadui kwasababu wanafanya hayo kwa faida ya wanakyela.

Mwisho, mwenyekiti alitoa pongezi kwa vikundi ambavyo vilileta bidhaa zao walizo tengeneza kupitia mikopo inayotolewa na halmashauri wakiwemo walemavu, ambao walitengeneza meza ya miti, na kinywaji kiitwacho Banana wine kutoka kwa wajasiliamali wengine ambacho kina nembo ya kyela, lakini pia kulikuwa na vikundi vya wanawake ambao walifuma mashuka. Pamoja na hayo mafunzo ya mikopo kwa vikundi vya ujasiliamali yaliendelea katika mamlaka ya mji mdogo wa kyela.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa