• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Lazima Tuibadilishe Kyela Kuwa Ya Kijani- Mhe. Juma Zuberi Homera

Imewekwa Kwenye: February 3rd, 2023

Haya yamezungumzwa leo tarehe 03/02/2023 na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Juma Zuberi Homera, alipokuwa akifanya uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti, zoezi lililofanyika katika viwanja vya shule Mpya ya sekondari Njisi iliyopo kata ya Njisi wilaya ya Kyela.

Amesema kwa kushirikiana na viongozi wa wilaya, wazee maarufu, mashirika na wadau wa mazingira tunao uwezo mkubwa wa kuifanya wilaya ya Kyela kuwa ya kijani kwa kupanda miti kila mahali.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma zuberi Homera akizungumza na wananchi kabla ya zoezi la upandaji miti.

Aidha Mheshimiwa Homera amesema ameamua kuja kufanya uzinduzi wa upandaji miti, ili kuhamasisha jamii kupanda miti, na baada ya uzinduzi wa zoezi hili, kila mwanafunzi atatakiwa apande miti 5, kisha tupande miti katika maeneo ya Zahanati, Hospitali ya wilaya pamoja na kwenye vituo vya afya. Na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetimiza agizo la Makamu wa Rais Mheshimiwa Mhe. Dkt. Philip Isidori Mpango.

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera akipanda mti ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti wilayani Kyela.

Katika suala la miundo mbinu, Mhe. Homera, amewaambia wanaKyela kuwa mkandarasi yupo njiani kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Njisi Itungi port ikiwa na taa za barabarani. lakini pia  amewataka wananchi kuendelea kusimamia mpango mzuri wa matumizi ya ardhi kwa maendeleo yao.

Aidha alitoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kwa kuikumbuka Kyela, na hata kuwajengea vituo vingi vya afya, pamoja na shule mpya nyingi ambapo wananchi na wanafunzi wameendelea kuapata huduma. Amesema kwa wanafunzi 5236 wa Mkoa wa Mbeya,  waliokosa nafasi ya  kujiunga kidato cha kwanza, watapelekwa katika vyuo vya ufundi ili kupunguza watoto wa mtaani, majina ya wanafunzi hao yatatolewa.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Keenja Manase akizungumza na wananchi wa kata ya Njisi kabla ya zoezi la uzinduzi la upandaji wa miti wilayani Kyela.

Nae Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine Keenja Manase, amewataka viongozi wa wilaya ya Kyela, kuendelea kushirikiana ili kuendeleza zoezi la upandaji miti katika wilaya yetu ya Kyela.

Mheshimiwa Josephine Keenja Manase Mkuu wa wilaya ya Kyela, (kulia) akipanda mti ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa upandaji miti katika wilaya ya Kyela.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi diwani wa kata hiyo Mhe. Omary Mwijuma amesema, maendeleo yanayoonekana leo ni nguvu ya serikali ya inayoongozwa na Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan, leo hii tunayaona madarasa ya kisasa kwenye kila shule.

Halmashauri ya wilaya ya Kyela imeweza kuitumia siku ya upandaji miti kwa kupanda miti 300, ikiwemo miti ya matunda, vivuli, mapambo na michikichi.

Mwisho.

Matangazo

  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Nafasi Za Kazi Tangazo Jipya January 01, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

    March 21, 2023
  • Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Afanya Kikao Kazi Na Watumishi Ili Kusikiliza Kero Zao

    March 17, 2023
  • Kamati Ya Siasa Ya Mkoa Wa Mbeya Imetembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Wilayani Kyela

    March 11, 2023
  • Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

    March 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa