Halmashauri ya Wilaya ya Kyela imeadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika katika Kijiji cha Lema Kata ya Busale tarehe 16.6.2025.
Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Kyela ambae ni Mgeni Rasmi Mhe.Josephine Manase ameishukuru Serikali ngazi ya Wizara kuweka mpango wa Taifa wa kuhakikisha vitendo vya ukatili kwa Wanawake na Watoto vinatokomezwa katika jamii.
Mhe.Manase amesema lengo la maadhimisho haya ni kukumbushana wajibu na majukumu yenye kuleta maendeleo ya Watoto.
Aidha Mhe. Manase amewaasa Wazazi kuwa mfano wa kuigwa kwa Watoto wao katika matendo mbalimbali pia amewataka Wazazi hao kuwa karibu na Watoto ikiwemo kuwapatia haki zote za Msingi ili kujua maendeleo yao pamoja na changamoto zinazowakabili.
Sambamba na hayo Mhe.Mkuu wa Wilaya amevitaka vyombo vya Ulinzi na Usalama kuhakikisha suala la Ukatili wa kijinsia linatokomezwa na kuchukuliwa hatua kali kwa watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.
Kauli mbiu Mtoto wa Afrika 2025 "Haki za Mtoto Tulikotoka Tulipo na Tuendako".
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa