• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: March 8th, 2023

Maadhimisho ya siku ya mwanamke yamefanyika tarehe 07/03/2023, katika kata ya Busale kijiji cha Lema hapa wilayani Kyela.

Maadhimisho hayo yameambatana na maonyesho ya kazi mbalimbali kutoka katika vikundi vya wajasiriamali pamoja na shuhuda za vikundi vilivyofanikiwa kubadili maisha yao ya umaskini hadi kuwa na maisha ya kawaida, baada ya kupata mikopo isiyokuwa na riba kupitia Halmashauri ya wilaya ya Kyela.

Akitoa hotuba yake wakati wa hafla hiyo, Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Keenja Manase amesema;

Amefurahishwa na maandalizi mazuri ya siku ya mwanamke yaliyofanyika katika kata ya Busale, ambayo yamejaa shangwe na bashasha kubwa.
Aidha ametoa shukrani nyingi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuijenga Tanzania pamoja na kumuokoa Mtanzania hususani mwanamke pamoja na makundi maalum kwa kutoa mikopo isiyokuwa na riba.

Pamoja na hayo Mhe. Mkuu wa wilaya amewataka wazazi kuwa mfano wa kuigwa katika familia zao na amekemea tabia za kupenda ngono, ulevi na matumizi ya madawa ya kulevya, kwani kwa kuacha tabia hizo, wazazi wanaweza pata muda wa kukaa na familia zao na kuzifundisha matendo mema.
Nae Afisa Mnadhimu wa jeshi la polisi mkoani Mbeya ndugu, christiner Msiyani amesema,

Anapenda kuwatia moyo wanawake wote kusimama kifua mbele, kwani wapo wanawake wenzao katika jeshi la polisi, wanaosimamia sheria bila kupindisha, hivyo wawe mstari wa mbele katika kutoa taarifa za unyasaji na ukatili wa kijinsia muda wowote wanapokutana na changamoto hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela, Ndugu Ezekiel H. Magehema, ametoa shukrani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuikumbuka wilaya ya Kyela, kwa kuleta fedha nyingi ambazo zimeibua miradi mingi ya maendeleo ambayo ni msaada mkubwa katika kutoa huduma kwa wananchi na kuwaletea maendeleo yao binafsi.
Mwisho.

Matangazo

  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Nafasi Za Kazi Tangazo Jipya January 01, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

    March 21, 2023
  • Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Afanya Kikao Kazi Na Watumishi Ili Kusikiliza Kero Zao

    March 17, 2023
  • Kamati Ya Siasa Ya Mkoa Wa Mbeya Imetembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Wilayani Kyela

    March 11, 2023
  • Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

    March 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa