Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Kyela Mhe.Emmanuel Bongo ameongoza mkutano wa Baraza kwa kipindi cha robo ya tatu katika ukumbi wa Mamlaka tarehe 2.6.2025.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya,Bi. Sabrina Hamoud amemshukuru Mwenyekiti pamoja na Wajumbe wa Mamlaka kwa ushirikiano mzuri na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo
Mhe.Bongo amesema kwa kipindi cha robo ya tatu Mamlaka imefanikiwa kukusanya jumla ya Tsh. Milioni 447,086,500.00 sawa na 75.11% ya makisio ya mwaka 2024/2025.
Aidha Mwenyekiti ameendelea kwa kusema kipindi cha robo ya tatu Mamlaka imefanikiwa kutoa Tsh. Millioni 44,708,650.00 sawa na 75.81% ya bajeti za 10% kwa ajili ya Wanawake,Vijana na watu wenye ulemavu.
Sambamba na hayo Mwenyekiti amesema katika kipindi cha robo ya tatu Mamlaka inatekeleza mradi wa jengo la kupumzikia abiria,pamoja na ujenzi wa zahanati ya Nkuyu.
Aidha Mhe.Mwenyekiti amempongeza Mtendaji Mkuu wa Mamlaka na Wataalamu wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kyela kwa jitihada kubwa ya ukusanyaji wa mapato na utendaji kazi katika idara zao.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa