Halmashauri ya Wilaya ya Kyela imenunua mtambo mpya wa kutengenezea barabara (scavator) kwa gharama ya Shilingi milioni 378 fedha za Mapato ya Ndani, ikiwa ni hatua muhimu katika kuimarisha miundombinu ya barabara hasa maeneo ya vijijini. Hatua hii imekuja baada ya juhudi madhubuti za usimamizi bora wa ukusanyaji wa mapato na matumizi yake chini ya uongozi thabiti wa viongozi wa Halmashauri hiyo.
Mtambo huo unatarajiwa kusaidia kwa kiwango kikubwa kazi ya ukarabati na uboreshaji wa barabara hasa kipindi cha mvua ambapo barabara nyingi huharibika na kuwa kikwazo kwa wananchi kufikia huduma muhimu kama shule, vituo vya afya na masoko ya kuuza mazao yao. Kupitia mtambo huo, barabara zitakuwa zinapitika wakati wote wa mwaka na hivyo kuchochea shughuli za kiuchumi vijijini.
Katika hatua nyingine, viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela wamesema kuwa ununuzi wa mtambo huu ni mwanzo tu wa jitihada za muda mrefu za kuboresha miundombinu. Wameeleza kuwa tayari mipango imewekwa ya kununua mitambo mingine ikiwemo Grader na roller zitakazosaidia katika utengenezaji wa barabara kwa kiwango bora zaidi na kwa ufanisi mkubwa.
Viongozi hao pia wametoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kulipa kodi na ushuru mbalimbali kwa hiari, wakisisitiza kuwa maendeleo haya yanatokana moja kwa moja na mapato yanayokusanywa kutoka kwao. Kwa ushirikiano huu, Kyela inaendelea kuwa mfano wa Halmashauri inayojitegemea na kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wake
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa