Mbunge wa jimbo la Kyela Mhe. Ally J. Mlaghila amemshukuru meneja wa RUWASA Kyela Eng.Tanu Deule kwa kupeleka wizara ya maji maombi ya kupewa mabomba ya miradi ya maji, na kufuatilia maombi hayo hadi kufanikiwa kuyapata, Shukrani hizo zimetolewa tarehe 12/06/2021, wakati wa upokezi wa mabomba hayo katika ofisi ya ujenzi halmashauri ya wilaya ya Kyela.
Akipokea mabomba hayo Mhe. Mbunge amesema, anamshukuru sana Meneja wa RUWASA Kyela Eng. Tanu Deule kwa kazi nzuri ya kuandika maombi katika wizara ya maji ili kupewa mabomba, Na siku ya leo tunapokea mabomba zaidi ya 700, yenye vipimo tofauti tofauti, ambayo yatafanya kazi katika miradi ya maji Kilombero, mradi wa maji wa Makwale, mradi wa maji wa Ngamanga group ikiwa ni pamoja na vijiji vyake vilivyokuwa havipati maji.
Aidha meneja wa RUWASA eng. Tanu Deule ametoa shukrani kwa viongozi wa wilaya akiwemo Mhe. Mbunge wa jimbo la Kyela, Katibu tawala wa wilaya ndugu Godfrey Kawacha, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ndugu Ezekiel H. Magehema, Pamoja na maafisa wote waliohudhuria tukio hilo kutoka ofisi za RUWASA na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela, Herry Willium Afisa tarafa ya Unyakyusa. Pia meneja huyo ameahidi kuyapeleka mabomba hayo haraka katika maeneo ya miradi ili kuanza kazi maramoja na kuwafikishia wananchi huduma ya maji.
Mwisho Mhe. Mbuge aliwaomba wananchi wa Kyela hasa wanaopitiwa na miradi hiyo, kujitokeze kwa wingi katika kazi za uchimbaji wa mitaro ya kupitishia mabomba hayo, na kuwaahidi kushirikiana nao katika zoezi zima la uchimbaji wa mitaro hiyo ili wananchi waweze kupata huduma ya maji kwa wakati.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa