• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkipata Mikopo Kaongezeni Mawazo Ili Mpate Kujikomboa - Katule G. Kingamkono

Imewekwa Kwenye: November 14th, 2022

Haya yamezungumzwa leo tarehe 14/11/2022 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkono alipokuwa akifungua mafunzo kwa vikundi 10 ambavyo vitapewa mkopo wa shilingi 110,000,000/=.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema, Halmashauri ya wilaya ya Kyela imekuwa ikitoa mikopo kwa vikindi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kila robo ya mwaka, kwa hiyo amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kutambua kuwa mikopo ya Halmashauri inatolewa kwa wananchi kwa kufuata taratibu na sheria ambazo zimewekwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kusaidia wananchi wake.

Aliendelea kwa kusema, Masuala ya utoaji wa mikopo yapo kisheria na ndio maana Serikali iliweka sheria ya kutoa mikopo yenye tija ili kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini na kujikwamua katika hali ya umaskini.

Pamoja na hayo, Mheshimiwa Katule amewaweka wazi wanavikindi kwa kuawaambia kuwa, fedha hizi zimetokana na mapato ya ndani ya Halamashauri, ambayo yamekusanywa na wataalam wetu wakisimamiwa na kiongozi imara Mkurugenzi Mtendaji ndugu Ezekiel H. Magehema hivyo ni lazima tuwapongeze lakini pongezi nyingi ziende kwa wananchi wenyewe ambao ndio walipa kodi.

Aidha aliwaasa wanabikundi kuwa na umoja mara baada ya kupata mikopo, na kuepuka migogoro. "Duniani kusingekuwa na migogoro basi hata hapa tulipo tungekuwa tupo paradiso" alisema Katule Kingamkono. 

hivyo aliwaasa vikundi kuepuka migogoro na wajenge umoja na ushirikiano ikiwa ni pamoja na kuongeza mawazo chanya ya kutanua mitaji wanayoipata kwa kupitia mikopo hii, ili kupata mafanikio katika maisha, na kutambua thamani ya mikopo hii inayoenda kutolewa na Halamashauri ya wilaya ya Kyela.

Pia alivitaka vikundi kujifunza kuweka akiba kwani akiba hiyo itakuja kuwasaidia pale wanapokwama, lakini kupunguza matumizi yasiokuwa ya lazima.

"Utajiri sio Ushirikina, Matamanio ya viongozi ni kuona mwananchi wa chini ananufaika na Serikali yao" ailisema Katule.
Aidha ameahidi  kwamba kwa kikundi chochote ambacho kitafanya vizuri katika marejesho na kupiga hatua ya maendeleo kwa mwaka, basi Halmashauri itakikopesha kikundi hicho shilingi 50,000,000/= ili kukiendelee kufanya vizuri na kuwa na mafanikio zaidi.

Akizungumza kwa niaba ya wanakikundi wenzake Grolia M. mwakibange ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka wananchi wote wa kipato cha chini ili kwa kupitia mikopo hii waweze kujiinua na kuongeza kipato katika familia zao.

Mwisho

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa