• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Zoezi la Ugawaji Wa Pikipiki 368 Kwa Maafisa Ugani Watendaji Kata Kimkoa Lafanyika Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: February 21st, 2023

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Juma Zuberi Homera, amegawa pikipiki 368 kwa niaba ya Mkoa wa Mbeya, ikiwa pikipiki 331 kwa maafisa Ugani na pikipiki 37 kwa watendaji wa kata, zoezi lililofanyika katika wilaya ya Kyela tarehe 21/02/2023.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa pikipiki hizo Mheshimiwa Mkuu wa mkoa amesema, Kwa maafisa wote na watendaji kata waliokabidhiwa pikipiki, wakazifanyie kazi iliyokusudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ili zilete tija kwa maendeleo ya wananchi.

"Twende tukafanye kazi ili tusimwangushe Rais wetu, na tuonekane tumetekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa mwaka 2020/2025" Amesema Mhe. Juma Zuberi Homera.

Pamoja na hayo mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amewataka maafisa ugani wote kwenda kusimamia kilimo na kufanya uzalishaji wenye tija, hasa katika zao la Mchikichi na mpunga kwa wilaya ya Kyela kwani mazao hayo yanalimwa kwa wingi hapa wilayani Kyela.

Kwa upande wa watendaji wa kata, Mheshimiwa Juma Zuberi Homera amewataka kwenda kuzitumia pikipiki hizo kwa kukusanya mapato na kuongeza asilimia ya mapoto yaliyokusudiwa katika kila wilaya.

Aidha Mheshimiwa Mkuu wa mkoa ametoa pongezi nyingi kwa wilaya ya Chunya kwa kukusanya 87% ya mapato hadi kufikia tarehe 19/02/2023, Pongezi kwa wilaya ya Kyela kwa kukusanya 71% ya mapato ambapo wilaya ilikusudia kukusanya mapato ya shilingi bilioni 4 lakini hadi sasa wilaya imekusanya bilioni 3, pongezi nyingine zilitolewa kwa halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa ukusanyaji wa 66% hadi kufikia sasa, amesema anaamini kwa kupitia pikipiki hizi mapato yataongezeka zaidi na kuvunja mafanikio ya mwaka wa fedha uliyopita.

Pia Mheshimiwa Homera ametoa shukrani zake za dhati kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela kwa kumpa nafasi ya kuzigawa pikipiki hizo kwa wilaya na kwa niaba ya mkoa mzima.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine Keenja Manase ametoa shukrani zake za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipatia wilaya ya Kyela pikipiki 49, na amewataka Maafisa wote na watendaji wa kata waliokabidhiwa pikipiki hizo kuzifanyia kazi ili ziweze kuleza maendeleo yenye tija kwa wananchi.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine Keenja Manase akiongea na maafisa Ugani na Watendaji Kata katika zoezi la ugawaji wa pikipiki

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkoni amewataka maafisa ugani na watendaji kata waligawiwa pikipiki, kuzitunza na ameahidi wao kama vionhozi watazisimamia pikipiki hizo na kuhakikisha zinafanya kazi iliyokusudiwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela ndugu, Ezekiel H. Magehema ametoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania jwa kutoa pikipiki 49 kwa wilaya ya Kyela, ambapo pikipiki 40 zitagawiwa kwa maafisa ugani na 9 kwa watendaji wa kata.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela ndugu Ezekiel H. Magehema akitoa taarifa za ugawaji wa pikipiki kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa

Amesema pikipiki hizo zinakwenda kusaidia katika ufanisi wa kazi hasa katika eneo la kilimo na eneo la ukusanyaji wa mapato, pamoja na hayo amesema pikipiki zilizogawiwa kwa watendaji kata zimezingatia ukubwa wa kata, umbali na ufanisi wa kata katika kukusanya mapato.

Mwisho maafisa ugani na watendaji wa kata wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuahidi kuongeza ufanisi wa kazi na kuto muangasha katika suala zima la kilimo na uongezaji wa mapato na kuleta maendeleo yenye tija kwa wananchi.

Afisa ugani wa kata ya Kajunjumele ndugu Everisto Mkwele akitoa shukrani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa niaba ya wenzake mara baada ya kupokea pikpiki.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa