Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Zuberi Homera amefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kuweka jiwe la Msingi katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kyela Cocoa Girls Secondary School tarehe 9.6.2025.
Katika ziara yake Mhe.Mkuu wa Mkoa Amefanya zoezi la ugawaji wa vipima unyevu vya zao la kakao 40 ambavyo huakikisha kuwa kakao zimekauka ipasavyo kabla ya kuhifadhi au kuuza,vyenye thamani ya Tsh.262,200,000/=ugawaji wa Mizani ya kidigitali 40 yenye thamani ya Tsh.116,000,000/=,kwa vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS), kukagua Ujenzi wa visima 5 vya maji vinavyogharinu Tsh.300,000,000,Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ya mfano ya Elimu ya awali na matundu sita ya vyoo katika Shule ya Msingi Mpanda.
Akizungumza na wafanyakazi wa KYECU LTD katika zoezi la ugawaji wa vipima unyevu Mhe.Homera amesema vifaa hivyo vitasaidia kudhibiti mianya ya udanganyifu pia amewataka viongozi hao kusimamia vizuri vyama vya ushirika kwani kupitia zao la kokoa Wilaya ya Kyela inakua kwa kasi kiuchumi.
Akikagua Mradi wa Maji Kijiji cha Mpunguti Kata ya Ikama Mhe.Juma Homera amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kuja na mpango wa kuchimba visima 900 Nchini ,kwani kati ya visima hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Kuna visima 5 ikiwemo kata ya Ikama Kijiji cha Mpunguti.
Mhe.Mkuu wa Mkoa ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela kwa ujumla kusimamia vyema fedha zinazoletwa na Serikali kwaajili ya Miradi ya maendeleo iliyopo katika Halmashauri.
Awali Mhe Mkuu wa Wilaya amemshukuru Mhe Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuweka mpango mzuri wa zao la kokoa kwani kupitia tozo ya Tsh.20 imesaidia kujenga Shule itokanayo na zao hilo na kukarabati Miradi ya maendeleo katika Sekta mbalimbalii.
Bomani Street
Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela
Simu ya Mezani: 025-2540035/7
Simu ya Mkononi: 0713655466
Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz
Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa