• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA KYELA AENDELEA NA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUZIPATIA UFUMBUZI KERO MBALIMBALI ZINAZOWAKABILI WANANCHI

Imewekwa Kwenye: July 14th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, ameendelea na ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Wilaya Kyela, ambapo leo tarehe 14.07.2025 amefika katika Kijiji cha Kilombero Kata ya Mababu.

Katika Ziara hiyo, Mhe. Manase ametilia mkazo umuhimu wa utunzaji wa mazingira, ambapo amewataka wananchi kuacha mara moja ukataji miti kiholela pamoja na shughuli za kilimo katika maeneo ya milima. Amesema kuwa tabia hizo zinaweza kusababisha mmomonyoko wa ardhi na maafa makubwa kama maporomoko ya ardhi au mafuriko.

Aidha, katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, DC Manase amewataka wananchi kuendelea kulinda amani. Ameonya dhidi ya kujiingiza kwenye siasa chafu ambazo zinaweza kuhatarisha utulivu na mshikamano tulionao, akisisitiza kuwa amani ni msingi wa maendeleo ya taifa lolote duniani. Vilevile, DC Manase amewaasa wananchi kuchagua viongozi wenye maono, watakaokuwa tayari kuleta maendeleo katika taifa letu na kuwa pamoja na wananchi katika shida na ra

Katika hatua nyingine, DC Manase amewahimiza wananchi kujiunga na Bima ya Afya ya Jamii (ICHF) kwa gharama ya shilingi elfu 30 kwa watu sita wa familia moja. Amesema kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kupunguza gharama za matibabu na kuhakikisha huduma bora za afya kwa kila mwananchi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Adv. Florah A. Luhala, alieleza kuwa tayari Halmashauri imeshapeleka shilingi milioni 30 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Kilombero, na ameahidi kukamilisha shilingi milioni 20 zilizobaki ili kuhakikisha shule hiyo inakamilika kwa wakati na kuwahudumia wanafunzi ipasavyo.

Pia akijibu kero ya uhaba wa nyumba za walimu, Adv. Luhala amesema kuwa Serikali kupitia halmashauri hiyo tayari imeanza ujenzi wa nyumba mbalimbali kwa walimu wa sekondari, ikiwemo Shule ya Sekondari Ibanda, Shule ya Sekondari Bondeni, na Shule ya Sekondari Mbeya Girls. Amesema kuwa mara tu bajeti ijayo Serikali itakapotoa fedha, halmashauri itashauri kuanza ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi ili kuboresha mazingira ya kufundishia kwa walimu katika ngazi zote.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AENDELEA NA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUZIPATIA UFUMBUZI KERO MBALIMBALI ZINAZOWAKABILI WANANCHI

    July 14, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA ISANGA WAPATA FARAJA KWA KUUNGWA MKONO NA MHE. DC MANASE KWA UANZISHWAJI WA UJENZI WA ZAHANATI

    July 12, 2025
  • TSH. MILLIONI TANO (5) KUTOKA MFUKO WA ZAO LA KAKAO KUSAIDIA UANZISHWAJI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA MSINGI KIJIJI CHA MPEGERE KATA YA MAKWALE

    July 10, 2025
  • WATAALAM WA AFYA KUTOKA MALAWI WAFANYA KIKAO NA WATAALAM WA AFYA KUTOKA KYELA KUJADILI NAMNA YA KUPAMBANA NA MAGONJWA YA MLIPUKO

    July 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa