• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Apongeza Idadi Kubwa Ya Wanafunzi Walioripoti Kujiunga Kidato Cha Kwanza Hapa Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: May 6th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kyela, Josephine Manase,amesema hadi kufikia Mei 3, mwaka huu, wanafunzi 189 waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza wilayani humo, bado hawajaripoti shuleni.

Amesema lakini licha ya changamoto hiyo, wanatakiwa wajipongeze kwani wanafunzi wengi wameitikia wito wa kwenda kuripoti kidato cha kwanza.

Mhe.Josephine aliyasema hayo wakati akitoa salamu zake katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kyela, kilichofanyika tarehe 04/05/2023 katika ukumbi wa halmashauri uliopo Kyela mjini.

Amesema wazazi ambao hawajawapeleka watoto wao kuripoti shule, tunaishi nao katika jamii, na wengi wao ukiangalia sababu wanazozitoa siyo za msingi, kwani Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewafanyia elimu bure sasa kwa nini wazazi wanakuwa wagumu, kutoa watoto kwenda kuhudhuria masomo darasani.

“Lakini pia sisi kama viongozi tujaribu kuongea na wazazi, na kuwaelimisha kwamba elimu ni muhimu kwa ajili ya watoto wetu, wanapopata elimu wao ndiyo wanaokuwa viongozi wetu wa baadaye, bila wao kupata elimu ina maana tunajenga taifa lisilokuwa na uwezo” alisema Manase.

Awali Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mheshimiwa Katule G. Kingamkono, amesema kutokana na Mradi wa ujenzi wa wodi ya Mama na mtoto kusuasua Baraza la Waheshimiwa Madiwani linatoa tamko kwamba mkurugenzi wa halmashauri Kyela, afanye maamuzi ya haraka kuvunja mkataba na TBA, Lakini kama TBA watarudi kazini kwa kasi waendelee, Ila kama wataendelea kusuasua wavunje mkataba mapema, sababu fedha ipo na kila kitu kipo ila kasoro yeye TBA, haleti mafundi kwa wakati .

Aliongeza ni aibu kwani Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, anahangaika kutafuta na kuwapelekea fedha lakini wao kama viongozi (madiwani), wanatakiwa kuweza kuzisimamia vizuri fedha hizo ili huduma ziweze kuwafikia wananchi.

“Utendaji kazi wa TBA siyo mzuri ndiyo maana tumetoa maelekezo, kama baraza na bahati nzuri niliutembelea mradi kama wiki moja iliyopita, na pia tulishawaambia TBA kama wataendelea kusuasua basi ni vizuri tuvunje mkataba, ili tuendelee kuweka taratibu nyingine” alisema Kingamkono.

Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri Kyela, Kenneth Nzilano, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuwasapoti kwa kutoa fedha nyingi, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali zikiwemo shule, madarasa, zahanati lakini pia hospitali ya wilaya hiyo.

Nzilano alisema ujenzi wa jengo la mama na mtoto katika hospitali ya wilaya, jengo lililoanza kujengwa mwaka 2020/2021, na jengo hilo kwa sasa lipo katika hatua za mwisho.

“Jengo halijaenda katika hatua ambazo zilikuwa zinahitajika, sababu ya ucheleweshwaji wa fundi mjenzi ambaye ni TBA, tumekaa naye kwamba kama hataweza kwenda na kasi tunayoitaka sisi, kama halmashauri ya kukamilisha jengo kwa wakati , basi tutafika mahali ambapo tutachukua hatua za kusimamisha mkataba wake” alisema Nzilano

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO AONGOZA MCHAKATO WAKUMPATA MAKAMU MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO NA WENYEVITI WA KAMATI ZA KUDUMU

    October 01, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI ADV. FLORAH A. LUHALA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MAPATO YA HALMASHAURI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    September 30, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA, MHE. JOSEPHINE MANASE, AMEKABIDHI HUNDI YA MFANO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA SITA HAMSINI NA TATU LAKI SITA (653,600,000/=) KWA VIKUNDI 70 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    September 22, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AFUNGA MAONESHO YA KUSINI INTERNATIONAL TRADE FAIR AND FESTIVAL YA MWAKA 2025

    September 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa